Mkuu wa wilaya akiondoka                  katika hosptali hyo mara baada ya kumalizika kwa kikao                  na watumishi .                                      Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.                 HALMASHAURI ya wilaya ya                      Hai,mkoani Kilimanjaro, imewasimamisha kazi                      watumishi wake wanne kwa tuhuma za kughushi hati za                      mishahara na kughushi nyaraka zilizofanikisha                      kuchukua jumla ya kiasi cha sh Mil 73.4 zikiwemo                      fedha za malipo ya muda wa kazi wa ziada kwa                      madaktari na wauguzi wa Hospitali teule ya Machame.                                                       Tuhuma hizo pia zina mtaja                      Mweka hazina wa Hosptali hiyo anayedaiwa                      kushirikiana na watumishi wa halmashauri hiyo                      kufanya ubadhirifu wa fedha na kwamba tayari Uongozi                      wa hosptali hiyo iliyo chini ya Kanisa la Kiinjili                      la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Kaskazini                      ,umekwisha  mfukuza kazi.                                                       Watumishi wawili kati ya                      wanne wamesimamishwa kazi kutokana na tuhuma mbili                      tofauti,moja ni kughushi hati za                      mishahara,vitambulisho na sahihi za watumishi                       waliostaafu  na wengine kuacha kazi na kuchukua                      mikopo wa Mil 35 katika benki ya CRDB kwa majina ya                      watumishi walioacha kazi.                |             
0 comments:
Post a Comment