Tunakujali, Tunakuthamini na Pia Tunakupenda!

Showing posts with label Michezo. Show all posts
Showing posts with label Michezo. Show all posts

July 18, 2014

  • TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI (TFF) LEO





    TAAFRIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI (TFF) LEO


  • NAHODHA WA UJERUMANI ASTAAFU KUCHEZEA TAIFA



    NAHODHA WA UJERUMANI ASTAAFU KUCHEZEA TAIFA

    Nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani Philipp Lahm amestaafu kucheza soka la kimataifa, baada ya kukiongoza kikosi chake na kushinda Kombe la Dunia nchini Brazil.Beki huyo wa Bayern Munich, ambaye pia anaweza kucheza kama kiungo, ameichezea Ujerumani mara 113.Lahm, 30, ataendelea kucheza Bayern Munich, ambapo amesaini mkataba hadi mwaka 


    2018. Habari za kustaafu kwake kuichezea timu ya taifa zimethibitishwa na chama cha soka cha Ujerumani DFB.

    Lahm alianza kuichezea Ujerumani Februari 2004 walipoichapa Croatia 2-1, na amestaafu kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Argentina katika fainali ya Kombe la Dunia.


  • DEL BOSQUE ATHIBITISHA KUENDELEA KUIFUNDISHA HISPANIA LICHA YA KUVURUNDA KOMBE LA DUNIA 2014


    DEL BOSQUE ATHIBITISHA KUENDELEA KUIFUNDISHA HISPANIA LICHA YA KUVURUNDA KOMBE LA DUNIA 2014
    Del Bosque confirms he will                  remain as Spain boss
    VICENTE del Bosque amevunja ukimya kuhusu hatima yake kwa kuweka wazi kuwa bado ana nia ya kuendelea kuwa kocha wa timu ya Taifa ya Hispania mpaka fainali za mataifa ya Ulaya mwaka 2016.
    Hispania iliboronga na kushindwa kutetea ubingwa wa dunia waliotwaa mwaka 2010 nchini Afrika kusini ambapo katika fainali za mwaka huu nchini Brazil walitolewa hatua ya makundi wakifungwa mabao 5-1 na Uholanzi na 2-0 dhidi ya Chile.
    Licha ya timu yake kufanya vibaya mwezi uliopita, Del Bosque amesisitiza kuwa hana nia ya kujiuzulu na anafurahi kuendelea kuisaidia Hispania.
    "Tunaweza kufanya mengi mazuri na kurudi kwenye mstari," kocha huyo mwenye miaka 63 aliwaambia waandishi wa habari nchini Hispania.
    "Tutajitahidi kutetea ubingwa wetu wa mataifa ya ulaya. Mabadiliko ya mfumo sio lazima, badala yake tunatakiwa kuendelea na mfumo wetu kwa kuongeza mabadiliko kidogo".
    Kocha huyo wa zamani wa Real Madrid aliyemrithi Luis Araggones baada ya ubingwa wa fainali za Euro 2008, aliiongoza Hispania kwa mafanikio katika fainali za mataifa ya ulaya za mwaka 2012 na za kombe la dunia mwaka 2010.
    "Nimekuwa katika mawasiliano na shirikisho wakati huu mgumu na wamefikiria kuwa mafanikio ya miaka sita iliyopita ni muhimu zaidi kuliko matokea mabaya katika mechi mbili," alisema Del Bosque ambaye mkataba wake unaisha mwaka 2016.
    "Shirikisho lina mtazamo chanya na wanathamini kazi yangu. Tunajiona imara na tutaendelea kufanya kazi yetu kama awali".

    "Tunajipanga vizuri  na tutafanya baadhi ya mabadiliko katika timu yetu kama tulivyofanya siku za nyuma".


  • July 13, 2014

  • KOCHA WA UJERUMANI AONYA, ASISITIZA REKODI MPYA KOMBE LA DUNIA LEO



    KOCHA WA UJERUMANI AONYA, ASISITIZA REKODI MPYA KOMBE LA DUNIA LEO
    Kocha Joachim Low, amesisitiza Ujerumani haimhofii Lionel Messi hata kidogo katika mechi ya fainali dhidi ya Argentina, leo.
    Lakini akasisitiza kuwa, Ujerumani itaweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza ya Ulaya kuchukua Kombe la Dunia katika ardhi ya Bara la Amerika Kusini.



  • July 12, 2014

  • FIFA YATANGAZA WATAKAOWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA



    FIFA YATANGAZA WATAKAOWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA
    Fifa imetangaza orodha ya majina 10 watakaowania tuzo ya mchezaji bora katika michuano ya Kombe la Dunia - 2014 Golden Ball.
    Wachezaji watatu wametoka Argentina, Angel Di Maria, Javier Mascherano na Lionel Messi. Mahasimu wao wa siku ya Jumapili Ujerumani, imetoa wachezaji wanne, Mats Hummels, Toni Kroos, Phillip Lahm na Thomas Muller.
    Wengine ni James Rodriguez kutoka Colombia, Neymar wa Brazil na Arjen Robben wa Uholanzi.
    Fifa pia imetangaza majina ya watakaowania tuzo ya golikipa bora wa michuano hiyo. Keylor Navas wa Costa Rica, Manuel Neuer wa Ujerumani na Sergio Romero wa Argentina watawania tuzo hiyo.
    Wakati huohuo Memphis Depay wa Uholanzi, Paul Pogba na Raphael Varane wa Ufaransa wamechaguliwa kuwania tuzo ya mchezaji bora chipukizi katika Kombe la Dunia.
    Washindi watatangazwa baada ya mchezo wa fainali siku ya Jumapili





  • July 09, 2014

  • In pictures: Brazil in shock over Germany defeat


    Brazil's 7-1 thrashing by Germany in the World Cup semi-final on Tuesday has sent shockwaves through the country, leaving fans of the host nation crushed.
    Brazilian fans react at the end of the semi-final football match between Brazil and Germany at on 8 July 2014.
    Brazil suffered their worst-ever World Cup defeat and first home loss in 12 years.
     Brazil fans watch the first half on Copacabana Beach during the 2014 FIFA World Cup semi-final match between Brazil and Germany on 8 July 2014
    Brazilians gathered in their thousands at Copacabana Beach in eager anticipation of the match...but the carnival atmosphere was not to last.
    Brazil fans watch the first half on Copacabana Beach during the 2014 FIFA World Cup semi-final match between Brazil and Germany on 8 July 2014 in Rio de Janeiro, Brazil.
    Fans were left stunned after Germany went 5-0 up in the first 29 minutes of play.
    Brazilian supporters react after defeat in the semi-final football match between Brazil and Germany on 8 July 2014
    Many had already left the Belo Horizonte stadium by the start of the second half.
    A Brazilian fan reacts while watching the 2014 FIFA World Cup semi-final match between Brazil and Germany on a public screen on the streets of Rio de Janeiro, Brazil on 8 July 2014
    For football fans and pundits in Brazil - a country built on sporting pride - the defeat came as a bitter shock.
    Crying Brazil fans while watching the first half on Copacabana Beach during the 2014 FIFA World Cup semi-final match between Brazil and Germany on 8 July 2014
    Smiles turned to tears on Copacabana Beach as Germany scored again and again.
    An emotional Brazil fan reacts after being defeated by Germany 7-1 on 8 July 2014
    After Tuesday's defeat, some Brazil fans have questioned whether hosting the tournament had been worth the cost.
    Brazilian supporters react after defeat in the semi-final football match between Brazil and Germany on 8 July 2014
    Dejected fans hung around the streets of Belo Horizonte in the hours after the game.
    Front pages of German newspapers showing photos from the FIFA World Cup 2014 semi-final football match between Germany and Brazil on July 9, 2014 in Berlin.
    German newspapers hailed the historic result. The front page of Bild, the biggest-selling paper in Germany, reads: "7-1. No words for it!"
    Football fans celebrate with a mock World Cup trophy in Duesseldorf, western Germany,on 8 July 2014
    A different atmosphere in Duesseldorf, Germany, where fans celebrated their team's victory into the early hours.
  • MANENO ALIYOTAMKA LUIZ FELIPE SCOLARI BAADA YA KUFUNGWA 7-1 NA UJERUMANI



    MANENO ALIYOTAMKA LUIZ FELIPE SCOLARI BAADA YA KUFUNGWA 7-1 NA UJERUMANI
    Luiz Felipe Scolari, kocha wa Brazil
    "Ni wakati mbaya zaidi kuwahi kutokea katika kazi yangu ya ukocha na siku mbaya zaidi katika maisha yangu ya soka. Lakini maisha yanaendelea. Nani anawajibika kwa matokeo haya? Ni mimi, ni mimi. Lawama za matokeo haya mabaya zinaweza kutuhusisha wote, lakini mtu aliyeamua timu ya kucheza na mbinu nilikuwa mimi.
    Lilikuwa chaguo langu. Tulijitahidi kufanya kila tuwezalo, tulicheza kwa kiwango chetu cha mwisho-lakini tumeishia dhidi ya timu kubwa ya Ujerumani. Hatukukata tamaa na kurudi nyuma. Tuliparaganyika na kupaniki baada ya kufungwa bao la kwanza na kila kitu kiliharibikia hapo. Hata Ujerumani hawawezi kuelezea ilitokeaje-lakini ni kwasababu ya ujuzi wao na unatakiwa kuheshimu hilo.

    Tunatakiwa kujiunza jinsi ya kukabiliana nalo. Ujumbe wangu kwa watu wa Brazil ni huu. Tafadhali watusamehe kwa kiwango hiki. Ninaomba radhi kwasababu hatujaweza kufika fainali-na tutajitahidi kushinda mechi ya nafasi ya tatu. Bado tuna sababu ya kucheza."


  • UJERUMANI YAICHAPA BRAZIL 7-1 NYUMBANI KWAO NA KUTINGA FAINALI



    UJERUMANI YAICHAPA BRAZIL 7-1 NYUMBANI KWAO NA KUTINGA FAINALI
    BrazilUJERUMANI imetinga Fainali ya Kombe la Dunia, baada ya kuwafumua wenyeji, Brazil mabao 7-1 katika mcheo wa Nusu Fainali uliofanyika Uwanja wa Mineirao mjini Belo Horizonte, Brazil.No way back: Oscar and Fred stand            ready at the centre circle with little hope of getting back            into the game
    Ujerumani inaingia Fainali kwa mara ya kwanza baada ya miaka 12- mara ya mwisho ilifungwa na Brazil katika fainali zilizoandaliwa kwa pamoja na Korea Kusini na Japan na sasa watamsubiri mshindi wa kesho kati ya Argentina na Uholanzi.



    Hadi mapumziko, tayari Ujerumani walikuwa mbele kwa mabao 5-0 yaliyofungwa na Toni Kroos mawili, Miroslav Klose, Thomas Muller na Sami Khedira. Brazil ilionekana wazi kuathiriwa na pengo la kuwakosa wachezaji wake tegemeo, beki na Nahodha Thiago Silva anayetumikia adhabu ya kadi za njano na mshambuliaji Neymar ambaye ni majeruhi, ambao nafasi zao zilizibwa na Bernard na DanteHistoric: The strike that made              hm the record holder.
    Ujerumani ilipata bao lake la kwanza dakika ya 11, mfungaji Thomas Muller baada ya makosa ya safu ya ulinzi ya Brazil.
    Miroslav Klose akafunga la pili dakika 23 baada ya kuukuta mpira uliopanguliwa na kipa Julio Cesar kufuatia shuti lake mwenyewe na kuandika bao lake la 16 kwenye Fainali za Kombe la Dunia akiweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi kwenye fainali hizo, akimpiku Mbrazil, Ronaldo Lima.Disbelief: Fernandinho,                  Maicon and David Luiz look bemused following Germany's                  fifth goal of the evening
    Toni Kroos akaifungia Ujerumani bao la tatu na la nne dakika za 24 na 26, kabla ya Sami Khedira kufunga la tano dakika ya 29. 
    Kipindi cha pili, kocha wa Brazil, Luiz Felipe Scolari alianza na mabadiliko, akiwatoa Fernandinho na Hulk na kuwaingiza Paulinho na Ramires, wakati mwenzake wa Ujerumani, Joachim Loew alimpumzisha Hummels na kumuingiza Mertesacker.Too easy! Eight Brazilians                  stand in the box as Muller finds space to guide the ball                  goalwards
    Mabadiliko hayo kidogo yaliiongezea uhai Brazil na kupeleka mashambulizi langoni mwa Ujerumani, lakini wakaishia tu kukosa mabao ya wazi.
    Ujerumani ikafunguka tena na kwenda kufunga mabao mawili zaidi, yote Andre Schurrle aliyeingia dakika ya 58 kuchukua nafasi ya Klose akimtungua kipa Julio Cesar dakika ya 69 na 79. Running riot: Germany scored                  four goals in six first-half minutes during Tuesday's                  semi-final against Brazil
    Brazil ilianya tena mabadiliko, Fred akimpoisha Willian dakika ya 69, wakati Ujerumani nayo ilimpumzisha Khedira nafasi yake ikachukuliwa na 
    Draxler dakika ya 76.
    Mesut Ozil alipata nafasi nzuri ya kufunga dakika ya 89, lakini akapiga nje na Brazil wakafanya shambulizi na kushitukiza na kujipatia bao la kufutia machozi lililofungwa na Oscar dakika ya 90.
    Wachezaji na mashabiki wa Brazil waliangua vilio baada ya mchezo huo, huku Wajerumani wakiangusha pati la maana uwanjani


  • July 05, 2014

  • STARS YA MART NOOIJ YATUA NCHINI KUTOKEA GABORONE




    STARS YA MART NOOIJ YATUA NCHINI KUTOKEA GABORONE

     Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


    TIMU ya Taifa ya Tanzania, Taifa stars  inatarajia kutua nchini kesho (julai 6) mwaka huu ikitokea nchini Botswana ili kuendelea na programu nyingine ya mazoezi.
     Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iliweka kambi ya wiki mbili, mjini Gaborone kwa ajili ya kujiwinda na mechi dhidi ya Msumbaji kuwania kupangwa hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika, AFCON mwakani nchini Morocco.
     Mechi hiyo muhimu kwa kocha wa Stars, Mholanzi, Mart Nooij itapigwa katika dimba la Taifa, julai 20 mwaka huu na wiki mbili baadaye mchezo wa marudiano utapigwa mjini Maputo nchini Msumbiji.
     Ikiwa ni sehemu ya kujipima ubavu, Stars ilicheza mechi ya kirafiki siku za karibuni na wenyeji wao Botswana na kuchapwa mabao 4-2.
     Mabao ya Taifa stars yalifungwa na Khamis Mcha `Vialli` na John Raphael Bocco `Adebayor`.
     Hata hivyo, matokeo hayo yalimfanya kocha Nooij ajue makosa ya kikosi chake na kuyafanyia kazi kabla ya kukabiliana na Black Mambas.
     Katika kambi ya Gaborone, Taifa stars ilimkosa winga wake machachari, Mrisho Khalfan Ngassa `Anko` aliyesafiri kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Free State Stars inayoyoshiriki ligi ya Afrika kusini.
     Kocha Nooij alimuita Ngassa ili acheze mechi ya kirafiki na Botswana, lakini ilielezwa kuwa nyota huyo alikaidi na kwenda kufanya majaribio katika klabu hiyo inayonolewa na Mbelgiji Tom Saintfiet.
     Taarifa za uhakika zinasema kuwa Nooij amemuengua Ngassa kuelekea mchezo dhidi ya Msumbiji na tayari nyota huyo yupo nchini baada ya kumaliza majaribio yake Afrika kusini ambapo alifuzu, lakini uhamisho wake bado ni tatizo.
     Msumbiji wana historia ya kuiharibia Taifa stars katika mechi muhimu, hivyo ni muhimu kwa kocha kukisuka kikosi chake pamoja na watanzania kuisapoti timu yao.
     Stars ilifanikiwa kufuzu raundi ya pili ya hatua ya awali baada ya kuifunga Zimbabwe bao 1-0 katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam na kulazimisha sare ya 2-2 mjini Harare nchini Msumbuji.
     Msumbuji wao walishinda mabao 5-0 mjini Maputo na kutoka suluhu pacha ya bila kufungana dhidi ya Sudani Kusini ugenini.
     Mshindi wa jumla katika mechi hiyo atafuzu hatua ya makundi  ya kusaka tiketi ya kucheza AFCON mwakani nchini Morocco.


  • GIGGS AWA DAKTARI WA SAYANSI...HESHIMA YAKO MKONGWE!



    GIGGS AWA DAKTARI WA SAYANSI...HESHIMA YAKO MKONGWE!
    Honour: The Manchester                        United legend poses with his degree at Victoria                        Hall in Bolton
    Heshima: Gwiji wa Manchester United akipozi katika picha baada ya kupata digrii yake kwenye ukumbi wa  Victoria Hall mjini Bolton.

    GWIJI wa Manchester United, amezawadia shahada ya heshima ya Udaktari na chuo kikuu cha Bolton kutokana na mchango wake mkubwa aliotoa katika mchezo soka.
    Giggs aliyestaafu kucheza soka mwishoni mwa msimu uliopita amepokea udaktari wa sayansi kwa mchango wake mkubwa katika michezo kwenye mahafali ya chuo iliyofanyika ukumbi wa Victoria Hall mjini Bolton jana ijumaa mchana. 
    Giggs anaongeza shahada hiyo katika shahada yake ya kwanza ya OBE aliyopata kutoka kwa Malkia mwaka 2007, shahada ya pili (MA) alipewa mwaka uliofuata na chuo cha Salford.
    Recognised: Giggs                        addressed graduate students at the university and                        congratulated them on their degrees
     Giggs aliwapongeza wanafunzi wa chuo kwa kupata digrii zao.


  • July 04, 2014

  • Algeria imerudi nyumbani kutokea Kombe la dunia


    Algeria imerudi nyumbani kutokea kombe la dunia
    algeria 2
    Kwenye kombe la dunia linaloendelea nchini Brazil, Algeria kutoka Afrika wameingia kwenye headlines zenye rekodi za kudumu kutoka kwenye mashindano haya baada ya kuwa moja ya timu mbili za Africa zilizogusa kwenye hatua nzuri kabla ya kutolewa.

    Tayari timu hii imerejea nyumbani Afrika ambapo kiukweli imepokelewa kwa shangwe sana, na naamini hata wengine wasio Waalgeria wangeipokea timu kama hii kutokana na ilichofanya.

    Algeria
    algeria 3
    algeria 4
    algeria 5
    Algeria


  • Musley Al Rawahi apania kufanya mambo makubwa Simba



    Musley Al Rawahi apania kufanya mambo makubwa Simba
    Musley Al Rawahi akisisitiza jambo.
    Mjumbe mpya wa kamati ya utendaji wa klabu ya Simba, Musley Al Rawahi, amesema kuwa silaha kubwa ya kufikia maendeleo katika klabu hiyo ni umoja na kufanya kazi kwa kujituma na uadilifu mkubwa.
    Musley ambaye mwaka jana alimzawadia gari kiungo wa Simba SC, Ramadhani "Messi" Singano kwa kucheza vizuri katika ligi kuu ya Tanzania Bara,  alisema hayo mara baada ya kutangazwa kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji wa klabu hiyo na pia kuwa miongozi mwa wajumbe wanaounda kamati ngumu na nyeti ya usajili wa klabu hiyo.
    Alisema kuwa anashukuru kuteuliwa kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji na usajili wa klabu hiyo na anaamini uteuzi wake umetokana na jinsi alivyokuwa mstari wa mbele kutafuta maendeleo ya klabu hiyo.
    Kwa mujibu wa Musley, Rais wa klabu hiyo, Evans Aveva hajafanya makosa katika uteuzi wa wajumbe wa kamati ya utendaji, usajili, mashindano na soka la vijana kwani hizo ndizo nguzo za ustawi wa klabu na kufanikisha mambo mengi ya maendeleo.
    "Tukisajili wachezaji wazuri, ndiyo watatuletea ushindi ndani ya klabu na hivyo kamati ya mashindano kufanyakazi zake kwa ufanisi mkubwa, hivyo natoa wito kwa wajumbe wateule, tufanye kazi kwa bidii na kuleta maendeleo makubwa klabuni na kuendelea kumpa sifa waliotuteua kushika nadhifa hizo," alisema Musley.
    Alisema kuwa yeye ana historia kubwa sana katika klabu hiyo na amekuwa mwanachama tangu akiwa mdogo na hiyo ilitokana na mapenzi makubwa ya baba yake kwa Simba.
    "Mzee wangu amekuwa mwanachama wa klabu hii kwa miaka mingi, mimi nimefuata nyayo zake na mpaka sasa nimekuwa na klabu hii kwa miaka mingi, nina uchungu nayo sana, ninaahidi kufanya kazi kwa bidii ili kufikia lengo," alisema Musley.
    Alisema kuwa changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni matarajio ya wanachama na mashabiki wa Simba kwani wanachotaka wao ni ushindi na kutwaa ubingwa.
    "Wana-Simba wanataka ubingwa, hakuna kingine ambacho wanakitaka, tunahitaji kusajili wachezaji wazuri, wenye kuleta ufanisi na kutufikisha kule tunakotaka," alisema.


  • July 01, 2014

  • SCHOLES ACHAMBUA USAJILI WA MAN UNITED …alia na Ander Herrera, amtaka Toni Kroos

     
     

    Against United: Kroos shields the ball from Danny Welbeck during a game at the Allianz Arena last season

    GWIJI wa Manchester United Paul Scholes anaamini kuwa klabu yake ilipaswa kumtupia jicho zaidi kiungo wa Bayern Munich Toni Kroos kwenye usajili wao kuliko Ander Herrera.

    Scholes anaona kuwa Herrera aliyesajiliwa kwa pauni milioni 28 hajafikia uwezo wa Kross anayeitumikia Ujerumani kwenye kombe la dunia.

    Scholes anasema kwa kumkosa Kroos, Manchester United itakuwa imepoteza nafasi ya kuwa na mchezaji mwenye kiwango cha hali ya juu.

    "Napenda kumtazama Kroos," anasema Scholes, "Nadhani ni mchezaji wa aina yake.

    "Napenda namna anavyomiliki mpira na anavyoudhibiti mchezo. Anaweza kutoa pasi na ana muono wa hali ya juu.

    "Kross anaweza pia kufunga kutoka nje ya box. Natamani Man United ingemsajili.

    Inafurahisha kuona United inasajili wachezaji wapya, lakini haijasajili mchezaji yeyote wa kiwango cha Kross."

  • FEYENOORD YAKIRI BEKI WAKE STEFAN DE VRIJ YUKO NJIANI KUTUA MANCHESTER UNITED

     

    On his way: Feyenoord believe Stefan de Vrij is destined for Manchester United in the coming weeks

    KLABU ya Feyenoord ya Holland inaamini kuwa safari ya mchezaji wake Stefan de Vrij kutua Old Trafford itakamilika wiki chache zijazo.

    Timu hiyo imejiweka tayari kumkosa beki huyo wa kati na tayari imeanza kuangalia mbadala wa nyota huyo wa miaka 22 anayeshiriki kombe la dunia na kikosi cha timu ya taifa ya Holland huko nchini Brazil.

    Vrij anaonekana atakataa ofa ya kujiunga na Lazio na badala yake dhamira yake ameielekeza United chini ya kocha Van Gaal kwa ada inayokisiwa kuwa ni pauni milioni 7.

    Kocha wa Feyenoord, Fred Rutten amesema: "Nilisaini mkataba wa kuitumikia Feyenoord kwa mazingira yoyote yale. Kama mchezaji anaondoka, hupaswi kuomboleza. Nina imani tutakuwa na nafasi nzuri ya kuziba mapengo."

  • SUAREZ AKIRI KUNG'ATA, AOMBA RADHI

     
    Luis Suarez amuomba radhi Chiellini
    Katika taarifa yake kwenye twitter amesema hivi:
    Baada ya siku kadhaa za kuwa nyumbani na familia yangu, nimekuwa na muda wa kutulia na kutafakari kuhusu hasa kilichotokea wakati wa mchezo kati ya Italy na Uruguay Juni 24 2014.
    Mbali na taarifa na zilizozagaa katika siku chache zilizopita, ambazo nyingi zimekuwa hazina nia ya kutatiza uwezo mzuri wa timu yangu ya taifa, ukweli ni kuwa, mwenzangu Giorgio Chiellini aliumia kutokana na mimi kumng'ata kutokana na kugongana na mimi. Kwa hilo:

    *Nasikitika sana kwa kilichotokea.
    *Ninamuomba rahi Giorgio Chiellini na familia yote ya wanasoka
    *Naahidi watu wote kuwa hakutakuwa na tukio kama hili tena
  • Ugiriki : Hatutaki Marupurupu yetu

     
     
     
     
    Hatutaki marupurupu yetu
    Huku timu za Afrika zikilazimika kusafirisha mamilioni ya dola za kimarekani hadi Brazil (Nigeria Cameroon) ilikuzima migomo kabla ya mechi muhimu timu ya Ugiriki ilifanya kinyume na hayo ilipokataa katakata kupokea malimbikizi ya marupurupu yao kutoka kwa serikali .
    Timu hiyo iliyoondolewa na Costa Rica katika mkondo wa pili ilimwandikia waziri mkuu wa Ugiriki Antonis Samaras barua ikimtaka atumie fedha hizo kujenga uwanja mpya wa kandanda utakaotumika k
    utambua na kukuza vizazi vipya vya kandanda.
    Ugiriki;Hatutaki marupurupu yetu
    Ugiriki iliambulia kichapo cha mabao 5-3 kupitia mikwaju ya penalti mikononi mwa Costa Rica.

    Bwana Samaras aliahidi kutekeleza ombi la wachezaji wake alipozungumza kwa njia ya simu na maafisa wa shirikisho la soka la Ugiriki.
  • ALGERIA YAPIGWA 2-1 NA UJERUMANI NA KUTOLEWA KOMBE LA DUNIA

     
     
     
     

    Mesut Ozil akishangilia baada ya kuifungia Ujerumani bao la pili
    AFRIKA imetolewa kabisa katika Kombe la Dunia baada ya wawakilishi wake waliobakia Algeria, kufungwa mabao 2-1 na Ujerumani katika mchezo wa 16 Bora usiku huu Uwanja wa Beira-Rio mjini Porto Alegre.
    Ni hitimisho la siku nyingine mbaya kwa Waafrika, baada ya awali, wawakilishi wengine waliofika hatua hiyo, Nigeria kutolewa na Ufaransa kwa mabao 2-0.Maana yake, Cameroon, Senegal na Ghana zinabaki kuwa timu zenye mafanikio zaidi miongoni mwa nchi za Afrika kwenye Kombe la Dunia kwa kuweza kufika Robo Fainali za michuano hiyo. Simba Wasiofungika walianza 1990 Italia, Simba wa Teranga wakafuatia 2002 Korea na Japan na Nyota Weusi wakamalizia 2010 Afrika Kusini. 
    Dakika 90 za mchezo kati ya Ujerumani na Algeria zilimalizika timu hizo zikiwa hazijafungana, lakini katika 30 za nyongeza mabao ya Andre Schurrle 92 na Mesut Ozil 119 yaliwafuta kabisa Waafrika katika Kombe la Dunia 2014 Brazil, mapema zaidi kuliko fainali zilizopita Afrika Kusini.
    Abdelmoumene Djabou aliifungia Algeria bao la kufutia machozi dakika ya mwisho kabisa, Ujerumani ikienda Robo Fainali.
    Kikosi cha Ujerumani kilikuwa; Neuer, Mustafi/Khedira dk70, Mertesacker, Boateng, Howedes, Lahm, Ozil, Schweinsteiger/Kramer dk109, Kroos, Gotze/Schurrle dk46 na Muller.
    Algeria: M'Bolhi, Mandi, Belkalem, Halliche/Bougherra dk98, Ghoulam, Lacen, Mostefa, Feghouli, Soudani/Djabou dk100, Taider/Brahimi dk79 na Slimani.
    Andre Schuerrle of Germany scores his team's first goal past goalkeeper Rais M'Bolhi of Algeria
    Andre Schuerrle akiifungia Ujerumani bao la kwanza dhidi ya kipa Algeria, Rais M'Bolhi
  • Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.