Polisi              katika nchi sita za Ulaya wamewakamata watu 17, kwa tuhuma              za kupanga mashambulizi.
        Watu hao wengi wao            wakiwa Wakurd wa Iraq, wanachama wa kundi la Wapiganaji wa            Kiislamu, wanadaiwa kwa kupanga mashambulizi nchini Norway na            Mashariki ya Kati.
        Katika kamata hiyo            polisi walililenga kundi la Rawti Shax, ambalo wamesema ni            kundi la waislamu wa dhehebu la sunni, ambalo limejikita            kuiondoa serikali ya Iraq katika jimbo la Kurdistan, na kuweka            utawala wa sharia.
        Polisi wamesema kundi hilo lilikuwa              likijiandaa kufanya mashambulizi ili kumuokoa kiongozi wake,              Muhubiri mwenye msimamo mkali ,Mullah Krekar anayeshikiliwa              nchini Norway.
        
0 comments:
Post a Comment