May 22, 2014

  • MCHUNGAJI ALIYEHARIBIWA SURA KWA TINDIKALI, SASA AENDELEA VYEMA

     
     
     

    Mchungaji Umar Umulinde wa Uganda akiwa hospitalini.

    Hizi ni baadhi ya picha alizopiga hivi karibuni mchungaji Umar Umulinde wa Uganda ambaye alimwagiwa tindikali katika mkesha wa sikukuu ya christmas mwaka jana mara baada ya kumaliza ibada,ambapo mpaka sasa kikubwa ambacho mchungaji Umulinde ambaye alikuwa muumini wa dini ya kiislamu kabla ya kubadili na kuokoka anasema ni kwamba waliomwagia tindikali ni waumini wa dini yake ya zamani kwani kabla ya kumwagiwa huyo mtu alisema neno linalotumiwa na waumini wa dini hiyo,ingawa kumekuwa na kuhusishwa kwa watu wengine kuhusiana na tukio hilo ingawa mchungaji huyo hataki kuamini.
    sura yake ndivyo inavyoonekana kwasasa.
    Mchungaji Umulinde.
    Ambapo mpaka sasa amekuwa akiuliza maswali mbalimbali kuhusiana na allah na Mungu wa biblia kama wana uhusiano wowote kwamaana Mungu wa biblia anayemuamini aruhusu mtu kuua ili akarithi mbingu kama allah anavyotaka,zaidi amewashukuru watu wanaoendelea kumuombea na kumtembelea hospitalini Kampala international ambako amelazwa akiendelea na matibabu pia sasa amewataka waumini wa dini ya kikristo kuendelea kuwaombea wenzao ili wamjue Mungu wa kweli kuliko kuendelea na malumbano nao kwakuwa hakutakuwa na faida yoyote.Bofya Kuangalia Picha zaidi>>>>>>>
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.