November 25, 2015

  • ONA JINSI UINGEREZA YALIVYO WAFURUSHA RAIA 500 WA NIGERIA>>>>!!!!!


    ONA JINSI UINGEREZA YALIVYO WAFURUSHA RAIA 500 WA NIGERIA>>>>!!!!!


    Image captionUingereza yawafurusha raia 500 wa Nigeria
    Ndege moja iliyokuwa imewabeba wahamiaji 500 raia wa Nigeria imetua mjini Lagos kutoka Uingereza.
    Wahamiaji hao 500 wametimuliwa na maafisa wa Uingereza baada ya kupatikana wakiishi nchini humo kinyume cha
    sheria.
    Image captionWengi wao wameelezea kutoridhishwa kwao na hatua ya kurejeshwa nchini Nigeria kwa nguvu.
    Wengi wao wameelezea kutoridhishwa kwao na hatua ya kurejeshwa nchini Nigeria kwa nguvu.
    Mmoja wao amemueleza mwandishi wa habari wa BBC aliyeko Lagos kuwa polisi nchini Uingereza walimkamata na kumfurusha mara moja pasi na kuma ruhusa ya kutwaa vitu vyake.
    Wachache kati yao ambao wamesema hawana jamaa mjini Lagos wamesalia katika uwanja wa ndege wasijue pa kwenda.
    Image captionNigeria inasisitiza inataka sheria zifwatwe kikamilifu kabla ya kutimuliwa kwa raia wake 29,000 kutoka Uingereza.
    Hivi majuzi serikali ya Nigeria ilielezea kutoridhishwa kwake na mpango ya utawala wa Uingereza ya kuwafurusha wahamiaji elfu thelathini 30,000 kutoka Uingereza.
    Nigeria inasisitiza inataka sheria zifwatwe kikamilifu kabla ya kutimuliwa kwa raia wake 29,000 kutoka Uingereza.
    Aidha Nigeria inataka Uingereza ihakikishe kuwa wale wanaorejeshwa ni wenye siha nzuri na wale wanaoweza kusafiri kwa ndege.
    Image captionNigeria inataka Uingereza ihakikishe kuwa wale wanaorejeshwa ni wenye siha nzuri na wale wanaoweza kusafiri kwa ndege
    Vilevile Nigeria inataka Uingereza ihakikishe kuwa wale wanaopelekwa Nigeria wanaasili na vyeti halali vya Nigeria na kuwa wanaweza kujishughulisha kimaisha kabla ya kuwarejesha Nigeria na kuwabwaga huko.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.