KITUO cha Uwekezaji            Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Kitengo cha viwanda vya            nguo katika Wizara ya Viwanda na Biashara, juzi kimepokea timu            ya wawekezaji ya VF Corporation kutoka Hong Kong.
        Taarifa iliyotolewa na            TIC jana, ilisema kituo hicho kimewataka wawekezaji hao            kuiangalia Tanzania kama eneo muhimu kwao kufanya uwekezaji            katika bara la Afrika kutokana na kuwa na mazingira na sera            rafiki ya kufanyia biashara.
        TIC imebainisha kuwa            Tanzania ina wananchi wapatao milioni 48, hivyo kuwa na soko            zuri kwa bidhaa zao na pia upatikanaji wa malighafi ni rahisi,            kuna nguvu kazi ya kutosha na jambo kubwa ni amani na utulivu            wa nchi.
        VF Corporation            iliyoanzishwa mwaka 1899, inaingiza kipato cha dola bilioni            12.3 na inajulikana kimataifa katika kutengeneza viatu na            vifaa vyake akiwa na bidhaa zaidi 30, washiriki wa biashara            60,000.
        Baadhi ya bidhaa            zinazotengenezwa ni mavazi ya jeans, michezo, viatu vya            michezo.
        Kwa sasa VF Corporation            inaagiza bidhaa katika kiwanda kimoja hapa nchini na            inaangalia uwezekano wa kupanua wigo wa manunuzi katika            viwanda vingine nchini.
        Katika ziara yao,            wawekezaji hao wamepitia upya mazingira ya uwekezaji nchini            kwa lengo la kuangalia uwezekano wa kuhamasisha viwanda vyao            vingine kuangalia Tanzania kama asili ya viwanda vya nguo.
        
0 comments:
Post a Comment