Askofu wa Kanisa la FPCT Jimbo la Tabora Kusini, Mchungaji Isaya Ilumba akimkabidhi mwanafunzi Nassoro Ally kiti cha magurudumu.
Mwanafunzi Nassoro Ally (miaka 10), wa              darasa la kwanza, Shule ya Msingi Chemchem akiwa na bibi              yake Joha Mhanuka baada ya kukabidhiwa kiti chake.
                Sabbas Prosper, mwanafunzi wa            darasa la kwanza  Shule ya Msingi Mlimwa B mkoani Dodoma akiwa            kwenye kiti alichopewa.
                Said Maganga wa Shule ya Msingi Chemchem,              Tabora akiwa kwenye kiti chake.
                Jeremiah Deo Deus (miaka 15) mwenye               ulemavu wa miguu na mikono baada ya kukabidhiwa kiti chake.
                Mtoto mwenye ulemavu, Sabbas Prosper              baada ya kukabidhiwa kiti cha kutembelea akiwa na maafisa              kutoka mkoani Dodoma.
                Mwanafunzi Nassoro Ally (miaka 10) wa              darasa la kwanza, Shule ya Msingi Chemchem, akiwa na bibi              yake, Joha Mhanuka ndani ya ofisi ya mwalimu mkuu akisubiri              kukabidhiwa kiti cha magurudumu.
        Kanisa            la Free Pentecostal Church of Tanzania (FPCT) kupitia mradi wa            kuwasaidia watoto wenye ulemavu nchini kwa msaada wa Shirika            Lisilo la Kiserikali la Sweden, ERIKS Development wamekuwa            mstari wa mbele katika kuwasaidia watoto wenye ulemavu ambapo            hivi karibuni walifanya tukio la kuwapa baadhi ya watoto hao            viti vya magurudumu 'wheel chairs'.
        Mratibu            wa mpango huo, Lucas Mhenga amesema kuwa dhamira ya FPCT na            ERIKS Development ni kuona watoto wenye ulemavu nao wanakuwa            na maisha mzuri kama wengine kwa kuhakikisha wanawasaidia            kadiri ya uwezo wao.
        "Tumekuwa            tukiguswa sana na changamoto zinazowapata watoto wenye ulemavu            na hivi karibuni tumekabidhi viti vya magurudumu kwa watoto            mbalimbali wenye ulemavu kutoka mikoa ya Tabora, Dodoma na            Arusha ili nao waweze kwenda shule kusoma bila shida ya            kusafiri," alisema Mhenga na kuongeza:
        "Tutaendelea            kufanya hivyo lakini tunahitaji sapoti, sisi wenyewe hatuwezi            kwa kuwa watoto hawa ni wengi na wana mahitaji mengi, kwa hiyo            tukiungana pamoja tunaweza kuwafanya nao waishi kwa amani na            furaha."
        Wakizungumzia            msaada huo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Chemchem iliyopo            Tabora, Hafsa Salum Juma na Mjumbe wa kamati ya shule, Yusufu            Juma Risasi ambao baadhi ya wanafunzi wao wamepata viti hivyo            walilishukuru sana Kanisa la FPCT kwa msaada wao.
        "Tunawashukuru            sana FPCT na ERIKS Development kwa namna ambavyo wamejitoa            kuwasaidia watoto hawa wenye ulemavu, kwa msaada wa viti hivi            watoto hawa wataweza kwenda shuleni bila usumbufu kwao na            wazazi wao.
        "Hii iwe            changamoto kwa watu wengine kuona wana jukumu la kuwasaidia            watoto hawa ambao bila kusaidiwa hawawezi kuishi maisha ya            furaha kama wengine," alisema Mwalimu Hafsa.
        Siku            chache baada ya watoto hao kupatiwa vifaa hivyo, mwalimu huyo            amesema mahudhurio yao yamekuwa mazuri na wanafunzi hao            wanafurahia masomo tofauti na ilivyokuwa huko nyuma.
        Wazazi wa watoto            wanasemaje?
                  Kufuatia msaada wa viti hivyo vya magurudumu kwa              watoto wenye ulemavu, wazazi wao wamesema, hawana cha              kuwalipa FPCT na washirika wake kwani wamefarijika sana na              wanaamini watoto wao watapata elimu katika mazingira rafiki.
        "Tulikuwa            tukipata tabu sana kuwabeba watoto wetu kuwapeleka shuleni,            kwenda na kurudi, hata walipokuwa shuleni walikuwa wakipata            tabu sana lakini baada ya kupewa viti hivi, ile adha            imeondoka. Tunawashukuru sana FPCT na ERIKS kwa misaada yao,"            alisema Joha Mhanuka, bibi wa Nassoro Ally aliyepata msaada wa            kiti.
        Naye            Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Manispaa ya Tabora, Robert            Kampambe alisema kuwa anawashukuru sana FPCT na ERIKS kwa            misaada yao kwani wameonyesha njia kwa wadau wengine            kuwasaidia watoto hawa.
        "Msaada wa FPCT na            ERIKS kwa watoto hawa walemavu ni changamoto kwetu hivyo natoa            wito kwa watu wengine ndani ya manispaa kuunga mkono jitihada            hizi. Tukiwaachia wao tu itakuwa mzigo mkubwa," alisema            Kampambe.
        
0 comments:
Post a Comment