November 26, 2015

  • BREAKING NEWS: SERIKALI YAPIGA MARUFUKU KUTENGENEZA NA KUCHAPISHA KADI ZA XMAS NA MWAKA MPYA KWA GHARAMA ZA SERIKALI


    BREAKING NEWS: SERIKALI YAPIGA MARUFUKU KUTENGENEZA NA KUCHAPISHA KADI ZA XMAS NA MWAKA MPYA KWA GHARAMA ZA SERIKALI
    Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amepiga marufuku utengenezaji na uchapishaji wa kadi za Christmas na Mwaka Mpya kwa gharama za serikali/umma, kwa mwaka huu.
    Balozi Sefue, ameelekeza kuwa yeyote anayetaka kutengeneza ama kuchapisha kadi hizo, afanye hivyo kwa gharama zake mwenyewe.
    Badala yake Balozi Sefue ameagiza fedha zilizopangwa kugharamia utengenezaji na uchapishaji wa kadi, zitumike kupunguza madeni ambayo Wizara, Idara na Taasisi za umma zinadaiwa na wananch/wazabuni waliotoa huduma na bidhaa kwao au zipelekwe katika matumizi mengine ya kipaumbele.

    Gerson Msigwa
    Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
    26 Novemba, 2015


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.