May 18, 2014

  • WAZIRI CHIKAWE AUNGANA NA MAAFISAWAKE KUSHANGILIA KUPITISHWA BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, BUNGENI DODOMA

     
     
     
     
     Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akipokea pongezi kutoka kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu, Mwamini Malemi (katikati) mara baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuipitisha Bajeti ya Wizara hiyo katika Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
     Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Haji Janabi (kushoto) akimpongeza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kulia) kwa kuyajibu kwa ufasaha baadhi ya maswali ya Waheshimiwa Wabunge na hatimaye Bajeti ya wizara hiyo ya Mwaka wa Fedha 2014/15 kupita. Kulia kwa Naibu Waziri Silima ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil na Naibu Katibu Mkuu, Mwamini Malemi.

     Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wapili kulia) akimfafanulia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, jinsi alivyoyajibu maswali ya waheshimiwa wabunge kabla ya kupitishwa Bajeti ya wizara hiyo ya Mwaka wa Fedha 2014/15.
    Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) wakipongezana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Pereira Ame Silima kwa kuyajibu maswali mbalimbali ya waheshimiwa wabunge na hatimaye Bajeti ya wizara yao kupitishwa na Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma. Nyuma yao, Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil na Naibu Katibu Mkuu, Mwamini Malemi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.