Serikali inatarajia kuweka                  katika mtaala wa elimu unaotumika sasa, somo la                afya ya uzazi kwa vijana katika shule za msingi na                sekondari nchini                kupunguza mimba za utotoni na maambukizi ya Ukimwi.Hayo yalisemwa                jana, Dar esSalaam na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Jenista                Mhagama katika ufunguzi wa mkutano wa siku tatu kuhusu 
                    serikali imeweka mikakati ya                  kuanzisha elimu hiyo ya afyaya uzazi na 
          jinsia kwa vijanakatika shule                  za msingi kutokana na ukubwa wa tatizo 
          la mimba za utotoni                  namaambukizi ya Ukimwi."Serikali inawahakikishia 
          wanasayansi kuwa elimu hiyo                  itawapa matokeo chanya kwamba hakutakuwa 
          na maambukizi wala mimba za                  utotoni kwa vijana hao,'' alisema Mhagama 
          katika hotuba yake ilisomwa                  kwa niaba yake na Mkurugenzi Msaidizi wa 
          masuala mtambuka katika wizara                  hiyo, Letisia Sayi.Mhagama alisema 
          elimu ya afya ya uzazi kwa                  vijana itasaidia kubadili tabia, kujikinga 
          kwa kutumia kondomu na                  wanaoishi na maambukizi kulinda afya zao.Naye, 
          Mtaalamu wa kitaifa wa masuala                  ya Ukimwi na elimu ya afya wa Shirika 
          la Elimu, Sayansi na Utamaduni                  (UNESCO), Martin Herman alisema takwimu 
          za wizara hiyo zinaonesha                  wanafunzi 6000 kila mwaka wanaacha shule kwa 
          sababu ya mimba za                  utotoni.Herman alisema mpango huo wa kutoa elimu ya 
          afya utaanza Julai mwaka huu                  baada ya mapitio ya mtaala huo na 
          inatarajiwa ifikapo mwaka 2015                  wanafunzi watajua afya ya uzazi na 
          kupata walimu waliobobea                  katika masomo hayo.Nchi zilizoshiriki mkutano 
          huo ni pamoja na Afrika                  Kusini, Kenya, Sweden, Uganda, Malawi, 
          Zimbabwe, Zambia, Burundi,                  Namibia, Rwanda, Botswana, 
          Lesotho,Swaziland,                  Angola, Ethiopia na wenyeji Tanzania
        
0 comments:
Post a Comment