May 28, 2014

  • MTAALA KUBADILISHWA KUPUNGUZA MIMBA ZA UTOTONI



    MTAALA KUBADILISHWA KUPUNGUZA MIMBA ZA UTOTONI

    Serikali inatarajia kuweka katika mtaala wa elimu unaotumika sasa, somo la afya ya uzazi kwa vijana katika shule za msingi na sekondari nchini kupunguza mimba za utotoni na maambukizi ya Ukimwi.Hayo yalisemwa jana, Dar esSalaam na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Jenista Mhagama katika ufunguzi wa mkutano wa siku tatu kuhusu 
    afya ya uzazi kwa vijana uliozishirikisha nchi 16.Mhagama alisema 
    serikali imeweka mikakati ya kuanzisha elimu hiyo ya afyaya uzazi na 
    jinsia kwa vijanakatika shule za msingi kutokana na ukubwa wa tatizo 
    la mimba za utotoni namaambukizi ya Ukimwi."Serikali inawahakikishia 
    wanasayansi kuwa elimu hiyo itawapa matokeo chanya kwamba hakutakuwa 
    na maambukizi wala mimba za utotoni kwa vijana hao,'' alisema Mhagama 
    katika hotuba yake ilisomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi Msaidizi wa 
    masuala mtambuka katika wizara hiyo, Letisia Sayi.Mhagama alisema 
    elimu ya afya ya uzazi kwa vijana itasaidia kubadili tabia, kujikinga 
    kwa kutumia kondomu na wanaoishi na maambukizi kulinda afya zao.Naye, 
    Mtaalamu wa kitaifa wa masuala ya Ukimwi na elimu ya afya wa Shirika 
    la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Martin Herman alisema takwimu 
    za wizara hiyo zinaonesha wanafunzi 6000 kila mwaka wanaacha shule kwa 
    sababu ya mimba za utotoni.Herman alisema mpango huo wa kutoa elimu ya 
    afya utaanza Julai mwaka huu baada ya mapitio ya mtaala huo na 
    inatarajiwa ifikapo mwaka 2015 wanafunzi watajua afya ya uzazi na 
    kupata walimu waliobobea katika masomo hayo.Nchi zilizoshiriki mkutano 
    huo ni pamoja na Afrika Kusini, Kenya, Sweden, Uganda, Malawi, 
    Zimbabwe, Zambia, Burundi, Namibia, Rwanda, Botswana, 
    Lesotho,Swaziland, Angola, Ethiopia na wenyeji Tanzania


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.