May 16, 2014

  • Wabunge 25 watarajiwa kuhama vyama vyao na kujiunga na chama kipya cha ACT-Tanzania.....Wamo wabunge 17 wa CHADEMA, Wanne wa CCM, Watatu wa NCCR-Mageuzi na mmoja wa CUF

     
     
     


    Wanasiasa  kutoka  vyama  mbalimbali  vya  siasa  nchini  wakiwemo  wabunge  17 kutoka  chama  cha  Demokrasia  na  Maendeleo  ( Chadema ),wanatarajiwa  kujiunga  na  chama  kipya  cha  siasa  nchini, ACT -Tanzania, kilichopata  usajili  wa  kudumu  mapema  mwezi  huu....


    Mbali  na  kuwanasa  wabunge  hao  wa  CHADEMA pia  kimefanikiwa  kuwavuta  wabunge  wanne  kutoka  chama  cha  Mapinduzi  ( CCM ),huku  kikiwa  na  uhakika  wa  kuwachomoa  wabunge  watatu  kutoka  NNCR-Mageuzi....

    Aidha  ACT- Tanzania  imepiga  hodi  ndani  ya  chama  cha  wananchi  (  CUF ) ,ambapo  imeshakamilisha  mchakato  wa  kumjuimuisha  kwenye  safu  yao  ya  mapambano  mbunge  mmoja  wa  viti  maalumu  wa  chama  hicho....

    Taarifa  za  uhakika    kutoka  ACT- Tanzania  zimeweka  wazi  kwamba  kwenye  idadi  ya  wabunge  17  wa  CHADEMA,wabunge  6  ni  wa  majimbo  huku  wabunge  11  wakiwa  ni  viti  maalumu.....

    Kwa  upande  wa  CCM,wabunge  watatu  watakaojiunga  na  ACT-Tanzania  ni  wa  majimbo,huku  mbunge  mmoja  akiwa  ni  wa  viti  maalumu.Ndani  ya  NNCR -Mageuzi, wabunge  wote  wanaotarajiwa  kujiunga  na  chama  hicho  ni  wa  majimbo  huku  baadhi ya  matawi  ya  chama  hicho  mkoani  Kigoma  nayo  yakitajwa  kuwa  katika  mchakato  wa  kugeuzwa  kuwa  ofisi  za  ACT-Tanzania....

    Katika kuhakikisha  chama  hicho  kinaenea  katika  kila  kona  ya  nchi,tayari  kimeshajiimarisha  kwenye  mikoa  ya  Kigoma,Rukwa,Katavi,Shinyanga,Lindi,Mtwara  na  Tabora  ambapo  viongozi  wengi  waliokuwa  wakikitumia  CHADEMA  kuanzia  ngazi  za  matawi  hadi  mikoa  wameanza  kufanya  kazi  za  ACT-Tanzania....

    Aidha  zipo  taarifa  kuwa  wapo  baadhi  ya  vigogo  wa    CCM  akiwemo  waziri  mkuu  wa  zamani  wanatarajiwa  kuwa  wanachama  wa  chama  hicho  na  kwamba  bado  kuna  mikakati  inafanyika  ili  kuhakikisha  chama  hicho  kinakuwa  chama  chenye  nguvu....
    Mmoja  wa  viongozi  wa  chama  cha  ACT-Tanzania  ambaye  hakuwa  tayari  jina  lake  liandikwe  kwa  madai  kuwa  si  msemaji  wa  chama  hicho,alisema  kwa  sasa  chama  kimeachwa  kwa  vijana  ili  kukisambaza  kwenye  kila  eneo  na  kwamba  muda  mwafaka  ukifika  kitaishangaza  nchi.....

    Tangu  kuanzishwa  kwake  mapema  mwaka  huu,ACT- Tanzania  kimeonekana  kuwa  chama  cha  upinzani  cha  kupambana  na  CHADEMA  tofauti  na  vyama  vingine  ambavyo  dhamira  zao ni    kuing'oa  CCM  madarakani....

    Chama  hicho  kimekuwa  kikiweka  matawi  yake  kwenye  maeneo  yanayotawaliwa  na  CHADEMA  mkoani  KIGOMA  na  kwenye  baadhi  ya  mikoa  nchini...

    Katibu  wa  ACT  kanda  ya  magharibi,Wiston  Moga  alinukuliwa  akisema  kuwa  lengo  la  chama  hicho  ni  kuleta  mabadiliko  kwenye  ulingo  wa  siasa, na  wao  wamedhamiria  kutetea  maslahi  ya  umma  kwa  lengo  la  kuondoa  mfumo  wa  maslahi   binafsi  ambao  ni  chachu  ya  vyama  vya  siasa  kushindwa  kuleta  mabadiliko  chanya  kwa  wananchi.....

    Msemaji  wa  CHADEMA,Tumain Makene  aliwahi  kunukuliwa  akisema  kuwa  hatua  ya  chama  hicho  kupingana  na  chama  chao  haina  mantiki  kwani  kinaonekana  kukosa  mwelekeo  mapema...

    "Tunajua  lengo  lao  ni  lipi, wanachokifanya  hakitawasaidia, ni vibaraka  tu  hao, nia  yao  ni  kuidhoofisha  CHADEMA, jambo  ambalo  hawataliweza" Alisema  Makene

    Kwa  upande  wake  katibu  mkuu  wa  ACT,Samson  Mwigamba  alisema  anaamini  ipo  orodha  ndefu  ya  wanachama  wa  vyama mbalimbali  vya  siasa  ambao  wako  tayari  kujiunga  na  chama  chao ...

    Mbali  na  Mwigamba, chama hicho  pia  kinaongozwa  na  Kadawi Limbu ( Mwenyekiti ),Ramadhani  Ramadhan  ( Makamu mwenyekiti )  na  Leopold  Mahona  ( Naibu  Katibu  mkuu )


    Source: Gazeti  la  Mtanzania
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.