June 22, 2014

  • FAIDA YA URAIA PACHA ? - DUGU MOJA, LAKINI NCHI TAFAUTI INAWEZEKANA KABISA.....


    FAIDA YA URAIA PACHA ? - DUGU MOJA, LAKINI NCHI TAFAUTI INAWEZEKANA KABISA.....
    Jerome (26) na Kevin-Prince Boateng (27)  ni ndugu wa baba mmoja kutoka Ghana na mama mbalimbali (Wajerumani) ambao wameweka historia ingine usiku huu kwa kucheza Kombe la Dunia pamoja lakini katika timu za nchi mbili tofauti. Jerome anachezea Ujerumani wakati nduguye Kevin-Prince anachezea Ghana, japo wote wamezaliwa Berlin, Ujerumani. 
    Usiku wa leo ndugu hawa wanaweka historia ya kucheza uwanja mmoja katika  timu tofauti wakati Ujerumani inacheza na Ghana. Mara ya kwanza walikutana kwa staili hiyo mnamo Juni 23, 2010 huko Afrika ya Kusini ambapo Ujerumani iliifunga Ghana bao 1-0. 
    Leo mpira umeisha kwa Ghana 
    na Ujerumani kutoka sare ya 2-2



  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.