May 12, 2014

  • Sifichi Hisia Zangu Nimempenda Kaka wa x Boy Wangu



    Jaman apa nshachanganyikiwa kabisaaa sijui kwa nini dunia hainipendi, jana nilienda Mliman city kutembea ghafla nkakutana na kaka wa aliyekuwa mchumba wangu ambae niliachana nae kama two weeks ago.

    Katika maongezi yetu akafurahi sana kuonana mie akaniomba nipate dinner pamoja nikamkatalia lakini aliniomba sana mwishowe nkaona any way siyo ishu, basi tukaenda somewhere for dinner.

    Baada ya dinner tukaanza kunywa wine na story kibao, mwisho wa yote akaniambia kuwa toka siku ya kwanza aliponiona na mdogo wake alinipenda, nimpe nafasi nikamwambia kwa sasa nina mpenzi mwingine ambaye ni (mkurya wangu niliyefahamiana humu humu)) akananipromis mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na kuninunulia gari ya kifahari.

    Nikamwambia anipe mda (ikumbukwe ana mke na watoto wa 2) basi tulikunywa sana mwishowe nikamuomba anipeleke nyumbani. Basi tukaingia kwenye gari acha aanze makisi romance sikuelewa chochote

    Tukaagana kwamba nitampa jibu leo, kuamka leo asubuhi kantext eti jana aliinjoy sana akinikosa atapata presha, sijamjibu lolote. Of course me huwa nipo wazi sifichi hisia zangu nahisi nampenda pia.

    Nishaurini nimpe jibu gani?


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.