May 09, 2014

  • MZAHA SAINGINE WATAKA PLAN

    Don't try It at home.

     MZAHA SAINGINE WATAKA PLAN Mdada mmoja alitaka kujua kiasi gani anapendwa na mume wake, hivyo akataka kujua mumewe atafanya nini endapo ataamua kuondoka na kumuacha! Mwanamke huyo akaamua kuandika barua inayosema "Samahani mume wangu, nimeamua kuondoka na kwenda kuanza maisha mapya mbali na wewe" Barua hiyo akaiweka juu ya meza iliyokuwa chumbani. Baadaye jioni, muda wa Mumewe kurudi mwanamke huyo akajificha chini ya uvungu wa kitanda mule chumbani Mume alipoingia chumbani akakuta ile barua juu ya meza, akaisoma kisha, akaandika maneno fulani kwenye ile ile barua, harafu akaanza kuimbaimba kwa furaha huku akipiga miluzi na akiwa anavua nguo.

    Akapiga simu na akasikika akisema hivi "hello mpenzi, nina raha sana leo.. yule mwanamke nuksi amesalenda mwenyewe kaondoka na kutuachia uwanja, jiandae nakuja" Muda huo huo Mume akaondoka. Mwanamke alipokuwa uvunguni akawa anatoka lakini amenyong'onyea na amelowa mashavu kwa machozi. Akasogea pale ilipo barua na akataka kujua mumewe aliandika kitu gani kwenye ile barua. Akakuta maneno haya "nimeona miguu yako uvunguni, tafadhali andaa chakula nina njaa sana mumeo, ila nimetoka kidogo nafuata maziwa nilisahau kupitia.

    Nakupenda mke wangu"
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.