Na Insp. Deodatus                Kazinja,PHQ
        Aliyewahi kuwa Kamishna                Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza Mzee Josephat                Mwingira aliyefariki tarehe 09 Juni, 2014 na kuzikwa                tarehe 12 Juni,2014 katika Makaburi ya Kunduchi Wilaya ya                Kinondoni Jijini Dar es salaam kwa heshima zote za                kijeshi.
        Marehemu Mwingira                aliajiriwa katika Jeshi la Magereza tarehe 11 January 1956                ambapo alianzia kazi katika Gereza Kuu Butimba la Jijini                Mwanza na maeneo mengine mengi nchini hadi alipo staafu                kwa mujibu wa sheria tarehe 01 Julai, 1990 akiwa                amelitumikia Jeshi la Magereza kwa miaka 33.
        Hayati Mwingira mbali na                kuwa kiongozi katika Jeshi la Magereza lakini pia alikuwa                kada maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na alishika                nyadhifa kadhaa enzi za siasa majeshi.
        Kamishana Jenerali wa                Jeshi la Magereza kwa niaba ya watumishi wote wa Jeshi la                Magereza anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki                kwa msiba huu mzito.
                Picha zote na Insp.                Deodatus Kazinja, Makao Makuu ya Magereza
        
0 comments:
Post a Comment