May 19, 2014

  • HII NDIO ADHABU ITAKAYOMPATA YEYOTE ATAKAETUMA PICHA ZA UCHI FACEBOOK NA TWITTER HUKO KENYA, CHEKI HAPA

     


    Ni kawaida sasa hivi kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na baadhi ya blogs na website kuweka picha za uchi au mitandao ambayo imekua maalum kwa ajili ya kueneza picha na video zikionyesha watu wakiwa uchi.
    Unaambiwa Kenya sasa hivi yeyote anaetuma msg zenye matusi au kusambaza picha za watu wakiwa uchi kwenye mitandao ya kijamii kama vile facebook na twitter atafungwa jela kwa miezi mitatu
    au kulipa faini ya zaidi ya shilingi laki tisa za Kitanzania.
    Kwa mujibu wa Radio Jambo, Mamlaka ya mawasiliano Kenya imetoa ripoti ikionyesha utumaji wa picha za watu wakiwa uchi na utazamaji wa mitandao ya ngono ulipanda kwa asilimia 60% mwezi April 2014 nchini Kenya.
    Unaonaje hii adhabu?
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.