May 26, 2014

  • MWANAMUZIKI MAARUFU AKAMATWA NA BANGI UWANJA WA NDEGE

    wizzz
    Rapa wa muziki wa nchini Marekani Wiz Khalifa amedakwa na polisi katika uwanja wa ndege mjini Texas baada ya kukutwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni bangi wakati wa zoezi la ukaguzi ndani ya mabegi yake.

    Staa huyo anayetamba na ngoma yake ya “Black and Yellow” alikuwa akisafiri kutoka El Paso kwenda Dallas wakati maafisa wa uwanja wa ndege walipokuta mzigo huo ndani ya begi lake ambapo kwa mujibu wa sheria aliwekwa kizuizini na baadae kufikishwa kituo cha polisi.

    Lakini Rapa huyo hakuonyesha kujali na baadae alitweet picha yake akiwa jela kuonyesha hasumbuliwi na hatua ya kukamatwa kwake.

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.