August 31, 2015

  • WAPIGANAJI 10 WA BOKO HARAMU WAUAWA CHAD


    WAPIGANAJI 10 WA BOKO HARAMU WAUAWA CHAD
    Image copyrightAFP
    Image captionWashukiwa 10 wa Boko Haram waliouawa Chad
    Wanachama kumi wa kundi la Boko Haram, wameuawa kwa kupigwa risasi nchini Chad.
    Wapiganaji hao walipewa adhabu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na vitendo vya kigaidi, katika kesi iliyofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo N'Djamena.


    Maafisa wa ulinzi wanasema kwamba waasi hao waliuawa na kitengo maalum cha ulinzi Kaskazini mwa mji mkuu.
    Washukiwa hao kumi walihukumiwa kuhusiana na mashambulio mawili yaliyotokea katika mji mkuu mwezi Juni, mwaka huu, mashambulio yaliyosababisha vifo vya watu 38.
    Lakini mwezi mmoja baada ya shambulio hilo, serikali ya Chad ilirejesha tena adhabu ya kifo, kwa washukiwa wanaopatikana na hatia ya ugaidi.
    Miongoni mwa waliouawa ni Mohamat Mustapha, anayejulikana kwa jina lingine kama Bana Fanaye, ambaye ametajwa kama kiongozi wa mashambulio ya Juni.
    Mahamat Mustapha
    Image captionMahamat Mustapha kiongozi wa mashambulio yaliyofanyika Juni nchini Chad
    Shule moja ya umma na kituo cha polisi kililengwa na walipuaji wa kujitolea waliokuwa kwenye piki piki, na kuwaacha zaidi ya watu mia moja na majeraha, mbali na waliouawa.
    Baada ya mashambulio hayo ya Juni, soko moja maarufu katika mji mkuu ulishambuliwa na watu kumi na watano kuuawa.
    Mashumbulizi hayo yalikuwa ya kwanza kuwahi kutekelezwa na wapiganaji hao kutoka Nigeria, nchini Chad ambayo inawahifadhi wanajeshi wa muungano ambao wanaendeleza harakati za kupambana na kundi hilo.
    Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka mkuu, Bruno Mahouli Louapambe, washukiwa hao walipatikana na hatia ya mashtaka kadhaa yakiwemo, njama ya kutekeleza uhalifu, mauaji, kuharibu mali kimakusudi wakitumia vilipuzi, ulaghai, kumiliki silaha na risasi bila idhini na kutumia bidhaa ambazo zinaweza kusababisha maangamizi.
    Chad imekuwa katika mstari wa mbele kuisaidi Nigeria, kuyakomboa maeneo yaliyotekwa na wapiganaji hao wa Boko Haram.
    Wanamgambo hao wa Kiislamu, ambao wanataka kuunda Jamuhuri yao ya Kiislamu nchini Nigeria, wamewauawa maelfu ya raia na kuwalazimisha mamilioni ya wengine kukimbia makwao Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo tangu 2009.
    Image copyrightBBC World Service
    Image captionRamani ya Nigeria
    Kundi hilo lilikuwa limetishia kushambulia Chad, baada ya serikali ya nchi hiyo kutuma wanajeshi wake nchini Nigeria, kupambana na kundi hilo na kukomboa maeneo waliyoyateka hasa katika jimbo la Borno.
    Kufuatia mashambulio hayo ya ,Chad ilipiga Marufu watu wote nchini humo kuvalia vitambaaa vinavyofunika nyuso zao, maarufu kama Burka.
    Lakini juhudi ya kudhibiti kundi hilo na ugaidi zimeshutumiwa na upinzani na makundi ya kutetea haki za kibinadam ambao wana wasi wasi kuwa huenda serikali ikahujumu haki za raia, kwa misingi ya kupambana na ugaidi.
    Image copyrightBoko Haram Video
    Image captionwapiganaji wa Boko Haram

    Wasifu wa Boko Haram

    • Boko Haram lilianzishwa mwaka wa 2002, dhamira kuu ikiwa kupinga mfumo wa elimu kutoka mataifa ya Magharibi. Boko Haram linamaanisha Elimu kutoka mataifa ya Magharibi imepigwa marufuku, kwa lugha ya Kihausa.
    • Kundi hilo lilianzisha operesheni za kijeshi 2009.
    • Maelfu ya watu wameuawa, wengi wao kutoka eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, wamewateka nyara mamia ya wengine wakiwemo wasichana 200 wa shule ya wasichana ya Chibok.
    • Iliijiunga na kundi la Islamic State na sasa limegeuza jina lake na kuwa Islamic State iliyo Magharibi wa Afrika au"West African province".
    • Boko Haram limeteka eneo kubwa Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, ambako limetangaza kuwa ni taifa huru la Kiislamu.
    • Wanajeshi wa Muungano hata hivyo wamefanikiwa kuyakomboa baadhi ya maeneo hayo.
    • BBC.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.