Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata              na kumfikisha mahakamani Daktari Feki Halima Sanga kwa kosa              la kugushi vyeti vya udaktari daraja la pili na kisha               kupangiwa kazi na wizara ya afya na ustawi wa jamii              Hospitali ya mkoa wa Ligula.
            
            
            
                                                   
                          
        Akizungumza                na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara                Henrry Mwaibambe amesema taarifa za mtuhumiwa huyo                ziliwafikia baada ya madaktari wa hospitali ya Ligula                kubaini mtuhumiwa huyo hafahamu mambo ya msingi ya                udaktari.
            Amesema                mtuhumiwa ambaye jina lake halali ni Halima Sanga, amekuwa                akitumia jina la Dr.Sara Matuja na aliajiriwa na wizara ya                afya 26-5-2015 na kufanya mazoezi ya udaktari katika                hospitali ya rufaa ya muhimbili kabla ya kupangiwa kazi                hospitali ya mkoa wa Ligula.
            Hata                hivyo kamanda Mwaibambe amesema baada ya Dokta.Sara Matuja                ambaye yuko hospitali ya rufaa ya Bugando, kupigiwa simu                alikiri  ni vyeti vyake na kudai huwenda mtuhumiwa                alivipata maeneo ambayo alivisambaza kuomba ajira,huku                akisisitiza uchunguzi unafanyika ili kubaini alipataje                kazi serikalini.
            Kamanda                amekiri binti huyo mwenye umri wa miaka 27 ni hatari                kutokana na matukio  ya nyuma ambapo gazeti la uwazi mwaka                2013 liliwahi kumkariri akisema aliyekuwa wazirimwanamke                huyo ni mtu hatari.
            ITV
          
0 comments:
Post a Comment