Kwa          watu wengi, pete ya dhahabu ni ishara ya upendo wa milele,          lakini mara nyingine simulizi nyuma ya dhahabu hiyo huwa si ya          kufurahisha sana.
        Tanzania          ni mzalishaji wanne wa dhahabu barani Afrika - lakini mamia ya          maelfu ya wachimbaji wadogo wadogo nchini humo hufanya kazi          katika mazingira magumu sana huku wakipata ujira mdogo na hata          kuwa na matumaini madogo ya mafanikio yao.
        Lakini          inawezekana hili likabadilika kufuatia mpango mpya ulioandaliwa          na shirika la Fairtrade kuuza dhahabu hiyo Uingereza - mpango          huu ni wa kwanza wa aina yake barani Afrika.
        Haya          ndio mazingira waliyonayo wachimbaji wadogo wadogo wengi nchini          Tanzania
        Lakini          kilomita moja kutoka hapa ni mgodi wa Nsagano.
        Mgodi          huu unatarajiwa kuwa mgodi wa kwanza Tanzania kuuza dhahabu          Uingereza chini ya mkataba wa fairtrade.
        Mkataba          huo unahakiksha ufuatialiaji wa vigezo vya afya na usalama          katika mgodi pamoja na malipo bora Zaidi.
        Akiinama          mbele ya beseni la blue ikiwa na maji yenye rangi la tope,          Prisca Alexi anavuruga matope ya malighafi ya dhahabu pamoja na          zebaki.
        Huku          akiwa amevaa glavui nyukundu mikononi mwake, anafanyakazi yake          ya kucheka mchanga huo na karai, akiwa makini maji hayo yasiguse          ngozi yake.
        Prisca          anafanya kazi kama mchekechaji, lakini anasema ujira anaoupata          ni mdogo mno.
        Mazingira          ya hapa ni duni sana, mbali na wachimbaji kuvaa fulana za kazi,          kofia ngumu na glavu.
        Alan          Frampton ni mkurugenzi wa Cred jewellery inayoiagiza dhahabu ya          fairtrade nchini Uingereza.
        Anasema          kuna uhitaji mkubwa kutoka kwa wateja kufahamu mazingira ambayo          bidhaa inatoka
        Lakini          mchambuzi wa maswala ya uchumi anasema aina ya mipango hii          inaweza kuharibu utaratibu wa kiuchumi wa biashara za ndani.
        Dr          Donald Mmari ni mkurugenzi wa utafiti na maendeleo katika          shirika la utafiti, REPOA
        'Huu          ni mpango pekee ambao unatarajiwa kunufaisha wachimbaji zaidi ya          200 katika mgodi mmoja, wakati ambapo wengi wao wengine          wataendelea kusota kwa maisha ambayo hayafanani kabisa na          wanachokichimba'.
        
0 comments:
Post a Comment