August 26, 2015

  • UKAWA WATAKA MAGUFULI AONGEZEWE ULINZI



    UKAWA WATAKA MAGUFULI AONGEZEWE ULINZI

    East Africa Radio
    Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar, Bw. Salum Mwalimu, amewataka CCM, kumwongezea ulinzi mgombea urais wao wa Jamhuriya Muungano, Dkt. John Magufuli ili asijiunge UKAWA. Alisema hivi sasa viongozi wa CCM wameimarisha ulinzi kwa makada wao wote maarufu ili wasijiunge UKAWA. "CCM wamwongezee ulinzi Dkt. Magufuli, wakimwachia dakika tano watasikia naye amejiunga UKAWA." Bw. Mwalimu aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika juzi Kibandamaiti visiwani Zanzibar. source: MAJIRA


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.