Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
HALI ya ugonjwa wa kipindupindu              imeanza kuzua hofu Dar es Salaam, Tanzania na kusababisha              kutolewa kwa amri ya kutouzwa chakula na matunda.
                Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,              Said Meck Sadick, leo ameawaambia waandishi wa habari kuwa              ni marufuku uuzwaji wa vyakula, matunda na hata kuhudhuria              katika misiba na matanga ya watu waliobainika kufa kwa              ugonjwa wa kipindupindu.
        Kwa mujibu wa Sadick, hadi sasa ni              watu 56 wamepatikana na ugonjwa huo baada ya kufanyiwa              vipimo.
        Ameyataja maeneo ambayo wagonjwa              hao wametoka kuwa ni Kjitonyama, Kimara, Makumbusho, Kigogo,              Manzese, Tandale na Mwananyamala katika Manispaa ya              Kinondoni.
        
0 comments:
Post a Comment