Mkurugenzi wa Mamlaka                  ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi amesema nchi za                  Afrika zina upungufu wa vifaa vya kutambua mvua                  zitakazonyesha kama ni El Nino.
                
                
                
              Kijazi alisema hayo                  jana alipokutana na wataalamu wa mamlaka ya hali ya hewa                  kutoka nchi za Afrika waliokutana kujadili na kuchukua                  hatua ya kukabiliana na majanga yatakayoambatana na mvua                  hizo.
              Dk Kijazi alisema                  wataalamu hao wanashindwa kuendesha kwa ufanisi shughuli                  za utabiri kutokana na vifaa kushindwa kutambua athari                  za mvua zitakazonyesha.
              "Tumekutana nchi 11 za                  Afrika ili kila nchi iweze kuchukua tahadhari ya mvua za                  El Nino... na tunasisitiza Serikali za nchi husika                  ziongeze vifaa vya kutosha vya kupima na kuchambua                  taarifa za hali ya hewa ili utabiri uwe wa ufanisi,"                  alisema Dk Kijazi.
              Alisema hadi jana                  kipimo cha utabiri wa hali ya hewa kilikuwa kinaonyesha                  joto halijaongezeka katika Bahari ya Hindi, endapo                  kutakuwa na mabadiliko watatoa taarifa ili Serikali                  ichukue tahadhari.
              Naibu Waziri wa                  Uchukuzi, Dk Charles Tizeba alisema mkutano huo unahusu                  mashirika ya hali ya hewa kutoka nchi za pembe za Afrika                  kujadili msimu wa mvua utakaoanza Septemba hadi Desemba                  mwaka huu.
              Dk Tizeba alisema                  watazishauri Serikali za nchi husika kuchukua tahadhari                  kwenye mamlaka za miji kuhusiana na mvua hizo.
              Alisema mabadiliko ya                  hali ya hewa yatagusa kwenye sekta ya miundombinu na                  kilimo, hivyo Serikali itajipanga kuchukua hatua.
              "Tunasubiri majadiliano                  ya wataalamu wa hali ya hewa yanayofanyika siku mbili                  watuambie cha kutufanya," alisema Dk Tizeba.
            
0 comments:
Post a Comment