May 21, 2014

  • Tumepata Tenda ha ha ha ha ha

    Blogu imepata tenda toka shirika la kimataifa kufanya utafiti ufuatao (tafadhali kama una jibu tusaidie tupate mkwanja):
    • Nchi gani ambapo wadada hawataki kupewa maua siku za Valentine na bethde zao?
    • Wapi ambako wazazi wote kila moja anadai alikuwaga wa kwanza darasani?
    • Wapi ambako unaweza kuwa na leseni ya udereva wakati hujawahi kushika usukani hata siku moja?
    • Wapi ambapo viongozi wa serikali hawajui kuimba wimbo wa Taifa?
    • Wapi ambapo wananchi wanaweza kukuua kwa kuiba kuku na wakakuabudu kwa kuiba mabilioni?
    • Wapi ambapo watu hugombania kuingia darasani, mpirani na hata kwenye mabasi?
    • Wapi ambapo kila unaekutana nae amewahi kuibiwa simu?
    • Wapi ambapo unaruhusiwa kulalamika kuwa ndugu zako wamekuroga kwa kila tatizo?
    • Wapi ambapo matajiri wote wana vitambi?
    • Wapi ambapo iPhone 5 zinauzwa kwenye foleni za magari kwa shilingi laki moja?
    • Wapi ambapo kupata dhamani polisi lazima ulipie?
    • Wapi ambapo basi la watu 25 linaweza kubeba watu 60.

    • Wapi ambapo ukimsindikiza mtu eapot, anaweza akafika South Afrika wakati wewe bado uko kwenye foleni hujafika kwenu?
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.