May 25, 2014

  • AFYA YA MH. VICKY KAMATA YAZIDI KUIMARIKA. NDUGU JAMAA NA MARAFIKI WAMIMINIKA HOSPITALINI KUMJULIA HALI.

    Na Steven Mruma.

         Hali ya Kiafya  ya Mh. Vicky Kamata aliyelazwa siku chache zilizopita, baada ya kuugua saa chache kabla ya Ndoa yake inazidi kuimarika huku ndugu jamaa na marafiki wakifika hospitalini kumjulia hali..
         Asubui na mapema nilifika tena hospitali na kukuta baadhi ya ndugu jamaa na marafiki waliofika hospitalini hapo kumjulia hali Mh. Vicky..
         Akiongelea afya yake Mh. aliendela kuwashukuru wote wanao muombea akiamini Mungu amesikia maombi yao na kwasasa hali yake imezidi kuimarika na anaweza kuruhusiwa wakati wowote kuanzia sasa.
    Baadhi ya ndugu zake [wadogo zake] waliofika kumjulia hali
    Mh. Vicky akiwa mwenye furaha baada ya kuwaona baadhi ya ndugu zake waliofika hospitali kumjulia hali
    Kwa ufupi hiyo suti nyeusi ikipambwa na shati jeupe na tai ya dhambarau ndio ilikua ivaliwe siku ya harusi ya Mh. Vicky Kamata. [Pembeni kulia ni mdogo wake Mh. Vicky akiwa na gauni la Dhambarau [pupple] ilikuwa ni sare ya harusi

    Mh. Ummy Mwalimu akiwa hospitali alipokuja kumuona rafki yake kipenzi Mh. Vicky Kamata
    Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na Mh. Vicky alipomtembelea hospitli mapema Leo
    Mh. A. Mshama nae alifika hospitali kumjulia hali rafki yake wa karibu Mh. vicky Kamata

    Ijapokuwa alikua Hospitali watu mbalimbali walifika na zawadi zao kuonyesha upendo

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.