June 25, 2014

  • MARCIO MAXIMO ASAINI MKATABA NA YANGA.



    MARCIO MAXIMO ASAINI MKATABA NA YANGA.

    index


    KOCHA Mkuu wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars Mbrazil,  Marcio Maximo anatarajia kuwasili nchini leo mchana akitokea kwao kwa ajili ya kuinoa timu ya soka ya Yanga iliyoanza mazoezi jana.
    kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Manyara Sports Management, Ally Mleh Maximo anawasili sambamba na msaidizi wake Leonardo Neiva.
    Ni kweli kocha Marcio Maximo amekubali kuingia mkataba na timu ya
    Yanga ambapo anatarajiwa kuanza kazi rasmi tarehe 27/06/2014 ambapo
    atafuatana na msaidizi wake Leonardo Neiva. Mazungumzo ya makubaliano
    hayo yalichukua muda mrefu kidogo hatimaye tumefikia
    makubaliano.Tunashukuru mungu kila kitu kimekamilika," alisema Mleh.
    Mleh alisema Manyara sports Management ni kampuni inayojishughulisha na uwakala wa
    wachezaji na makocha, kutafuta wadhamini katika michezo, na usambazaji
    wa vifaa vya michezo.
    Alisema kwa niaba ya Marcio Maximo anapenda kuushukuru uongozi wa klabu ya
    Yanga, kwa kweli wameonyesha  umakini na professional kwa muda wote wa
    majadiliano. Nawaomba wachezaji,wanachama na wapenzi wote wa Yanga
    wampe ushirikiano.
    Baada ya kumaliza mkataba wake wa kuifundisha Taifa Stars nchini
    aliingia mkataba na timu kubwa nchini Brazil  mpaka mkataba wake
    ulipoisha.Kwa wakati huu kulikuwa na mazungumzo na timu mbalimbali
    Zilizotoa  ofa nchini China, Ethiopia na Afrika kusini lakini Yanga
    wamefanikiwa kumnasa kocha huyo.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.