June 30, 2014

  • WATANZANIA WAENDELEA KUMIMINIKA KATIKA BANDA LA PPF SABASABA KUJIPATIA HUDUMA MBALIMBALI



    WATANZANIA WAENDELEA KUMIMINIKA KATIKA BANDA LA PPF SABASABA KUJIPATIA HUDUMA MBALIMBALI
     Afisa Michango kutoka PPF Makao Makuu, Bi Glory Maboya (kulia) akimpatia maelezo ya Huduma mbalimbali mmoja wa wateja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakati alipotembelea Banda la PPF katika Viwanja vya Mwl Nyerere maarufu kama Sabasaba.
     Mkazi wa Jiji la Dar Es Salaam akipatiwa maelezo juu ya huduma ya Fao la Kujitoa kutoka kwa afisa uendeshaji wa Mfuko wa PPF kanda ya Ziwa, Bi Grace Balele wakati mteja huyo alipotembelea banda la Mfuko wa Pensheni wa PPF katika Maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya Sabasaba.
    Mchambuzi wa Mfumo wa Teknolojia (System Analysist) kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF Makao Makuu, Bi Irene Togolai akimpatia fomu ya Kujiunga na Mfuko wa Pensheni wa PPF mmoja wa Wakazi wa Jiji la Dar aliyetembelea Banda la PPF katika Maonyesho ya 38 ya Kibiashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba
    Mchambuzi wa Mfumo wa Teknolojia (System Analysist) kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF Makao Makuu, Bi Irene Togolai akijibu maswali ya wateja wa PPF waliofika katika banda la PPF katika Maonyesho ya 38 ya Biashara za Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwl Nyerere Barabara ya Kilwa, Jijini Dar Es Salaam.
     Happiness Mmbando , Afisa Rasilimali watu Utawala na Ushauri kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF akiwasikiliza kwa makini baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar waliotembelea Banda la PPF katika Maonyesho ya 38 ya Biashara za Kimataifa.
    Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar Es Salaam wakiuliza maswali kuhusiana na mfuko wa Pensheni wa PPF wakati walipotembelea katika banda la PPF katika Maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar Es Salaam, Kulia ni Afisa Huduma kwa Wateja Kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF kanda ya Temeke, Bi Jacquline Jackson


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.