June 26, 2014

  • TBL kuwajengea Kisima cha maji cha Sh Mil. 29 wananchi wa Saranga, Dar

     
     
     
     

    Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dorris Malulu akimkabidhi Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa King'ongo, Benetris Mapesi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. mil 29  za msaada wa ujenzi wa kisima cha maji katika mtaa huo uliopo Kata ya Saranga, Kinondoni Dar es Salaam. Hafla hiyo ilifanyika katika mtaa huo mwishoni mwa wiki.Wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni Mkandarasi wa kisima hicho, Onesmo Sigala (wa pili kulia) wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya MO Resources Limited,na Mjumbe wa Kamati ya Maji ya Mtaa wa King'ongo, Anna Kibwana ( wa pili kushoto).

    Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dorris Malulu akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya ukandarasi ya MO Resources Limited, Onesmo Sigala (kulia) mfano wa hundi yenye thamani ya sh. mil 29  za msaada wa ujenzi wa kisima cha maji katika mtaa huo uliopo Kata ya Saranga, Kinondoni Dar es Salaam. Hafla hiyo ilifanyika katika mtaa huo mwishoni mwa wiki.Wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni Mjumbe wa Kamati ya Maji ya Mtaa wa King'ongo, Anna Kibwana (wa pili kushoto),Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa King'ongo, Benetris Mapesi.

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.