June 26, 2014

  • UFARANSA, USWISI ZAPETA HATUA YA 16 KOMBE LA DUNIA,

     
    TIMU ya Taifa ya Ufaransa imefuzu hatua ya 16 ya kombe la dunia kama washindi wa kwanza wa kundi E baada ya usiku huu kuambulia pointi moja kufutia suluhu ya bila kufungana na Ecuador.
    Ufaransa wamefikisha pointi 7 kileleni wakifuatiwa na Uswisi wenye pointi 6 katika nafasi ya pili baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Honduras.
     
    Mabao yote ya Uswisi yamefungwa na Xherdan Shaqiri katika dakika ya 5, 30 na 70.Kwa matokeo hayo, Ecuador waliomaliza katika nafasi ya nne kwa pointi 4 na Honduras walioshika mkia bila pointi yoyote wameaga rasmi mashindano ya mwaka huu ya kombe la dunia.
     
    Kikosi cha Ecuador: Dominguez, Paredes, Guagua, Erazo, Walter Ayovi, Antonio Valencia, Minda, Noboa (Caicedo 89), Montero (Ibarra 63), Arroyo (Achilier 82), Enner Valencia.
    Wachezaji wa akiba: Banguera, Mendez, Rojas, Jaime Ayovi, Bagui, Saritama, Martinez, Gruezo, Bone.
    Kadi ya njano: Erazo.
    Kadi nyekundu: Antonio Valencia.
    Kikosi cha Ufaransa: Lloris, Sagna, Koscielny, Sakho (Varane 61), Digne, Griezmann (Remy 79), Pogba, Schneiderlin, Matuidi (Giroud 67), Sissoko, Benzema.
    Wachezaji wa akiba: Ruffier, Debuchy, Evra, Cabaye, Cabella, Valbuena, Mavuba, Mangala, Landreau.
    Mwamuzi: Noumandiez Doue (Ivory Coast)
    Kikosi cha Honduras: Valladares, Figueroa, Bernardez, J Garcia, W Palacios, Bengtson, Costly, B Garcia, Espinoza, Claros, Beckeles.
    Kikosi cha Switzerland: Benaglio, Lichtsteiner, Inler, Xhaka, Behrami, Rodriguez, Mehmedi, Drmic, Djourou, Schaer, Shaqiri.
     
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.