June 30, 2014

  • RATIBA YA RAMADHAN LEICESTER UK


    RATIBA YA RAMADHAN LEICESTER UK
    Assalaamu Alaykum,
    Jumuia ya Kiislamu ya An Noor ya Leicester Uingereza inapenda kuwatakia
    Waislamu wote mfungo mwema wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
    Allah akujaalieni nyote afya na nguvu za kutekeleza ibada nyingi zaidi ndani Ya Mwezi huu Adhimu. Pia awape Shufaa ndugu zetu wenye matatizo ya Kiafya na mengineyo. Amin

    Jumuia ya An Noor inapenda pia kuwatangazia Waislamu wenzao waishio Leicester Na vitongoji vya karibu kuwa Programu ya Ramadhan InshaaAllah
    Itaendelea kama kawaida mwaka huu kwa utaratibu wa Kawaida.
    Kila Jumamosi na Jumapili kutakuwa na Darasa za Mwezi wa Ramadhan
    Kuanzia Saa Moja na Nusu jioni katika jengo letu 170a Belgrave Gate LE1 3XL Leicester
    Baada ya hapo tutakuwa na Futari ya pamoja.
    Kama kawaida kila Familia itashiriki katika kuleta futari
    Kadhalika kila Familia inakumbushwa kuchangia £5 kila wiki kwa ajili ya Maandalizi.
    Programu InshaaAllah itaanza Jumamosi 5/7/2014.
    Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na hawa wafuatao:

    Malik 07983614261 au ust Farid 07792174408
    au tutumie email: madrasatulnoor.01@gmail.com
    Kullu Am Wa Antum Bikhayr


    Mohammed Omar, 
    Mwenyekiti wa Jumuia 


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.