June 25, 2014

  • Picha Kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa:Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe Ashiriki Kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika, Malabo, Equatorial Guinea



    Picha Kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa:Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe Ashiriki Kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika, Malabo, Equatorial Guinea
     Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania akitoa mchango wa Tanzania kwenye Kikao cha Mawaziri wa Umoja wa Afrika. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na kwenye Umoja wa Afrika Mhe. Naimi Aziz na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhe. Christopher Chiza wakifuatilia mchango huo kwenye mkutano unaoendelea Mjini Malabo Equatorial Guinea tarehe 23-24 Juni 2014.
    Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifuatilia majadiliano ya vikao vya wataalam kabla ya Kikao cha Mawaziri kuanza. Wengine pichani ni maafisa wa Mambo ya Nje Sam Shelukindo, Elisha Suku  na Zuleha Khamis.
    Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa kwenye mazungumzo ya faragha na Mawaziri wenzake wa Mambo ya Nje wa Botswana (juu) Mhe. P.T.C. Skelemani na (chini) Mhe. Netumbo Nandi Ndaitwah wa Namibia pembezoni mwa mikutano ya Mawaziri wa Umoja wa Afrika Mjini Malabo, Equatorial Guinea tarehe 23-24 Juni 2014.
    chanzo haki ngowi.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.