June 08, 2014

  • MBEYA CITY FC ZITENDEENI HAKI MILIONI 360 ZA BINSLUM, FANYENI HAYA KUKIMBIA `USWAHILI` WA SIMBA, YANGA



    MBEYA CITY FC ZITENDEENI HAKI MILIONI 360 ZA BINSLUM, FANYENI HAYA KUKIMBIA `USWAHILI` WA SIMBA, YANGA
    Binslum-2Na Baraka Mpenja wa fullshangwe, Dar es salaam
    0712461976
    MBEYA CITY FC kwa mara ya kwanza imepata udhamini wa mamilioni ya fedha baada ya Kampuni ya Binslum Tyre Company Limited kumwaga kitita kirefa cha milioni 360 kwa miaka miwili.
    Kampuni hii ina nia ya kuifanya klabu hii kuwa bora zaidi katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara . Siku zote ukifanya kazi kwa moyo wote, ukawekeza nguvu kubwa kutafuta mafanikio, mwisho wa siku juhudi zako zinakulipa.
    Msimu uliopita, Mbeya City walionesha nguvu kubwa na mipango mizuri ya ndani na nje ya uwanja. Walicheza kwa kujituma, kwa malengo na nidhamu kubwa. Timu hii ilikuwa bora kuliko timu zote tatu zilizopanda ligi kuu kwa msimu uliopita.
    Ashanti United na Rhino Rangers ziliishia kuonja tu utamu wa ligi kuu na kurudi tena ligi daraja la kwanza. Lakini kwa Mbeya City fc ilikuwa ni tofauti, walishindana mpaka dakika ya mwisho na kumaliza katika nafasi ya tatu.
    Waliwachomoa wakongwe, Simba sc katika ushindani wa nafasi tatu za juu. Nidhamu ya wachezaji na kuwa na uchu wa mafanikio, maandalizi ya muda mrefu, falsafa ya kocha Juma Mwambusi, hamasa ya mashabiki, uongozi wenye mipango, ni miongoni mwa sababu chache kati ya nyingi zilizowafanya Mbeya City wafike pale walipo.
    Lakini kilio chao kilikuwa ni kukosa udhamini. Viongozi walisikika mara nyingi wakisema wanaomba makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini klabu. Haikuwa rahisi kupata udhamini kwasababu ndio kwanza watu walikuwa wanapima upepo wake.
    Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.