June 22, 2014

  • Kauli ya Uganda baada ya kuwekewa vikwazo na Marekani kwa kupinga ushoga



    Kauli ya Uganda baada ya kuwekewa vikwazo na Marekani kwa kupinga ushoga

    Katibu mkuu wizara ya mambo ya nje wa Uganda, Balozi James Mugume, 
    amesema kuwa Uganda haitishwi na vikwazo ilivyowekewa na Marekani kama 
    hatua ya kupinga sheria yake kali kuhusu Ushoga.Kwa mujibu wa BBC, 
    Balozi Mugume ameelezea kuwa serikali ya Uganda hata hivyo itafanya 
    mazungumzo na Marekani ili kufafanua hatua waliyochukua.Amesisitiza 
    kuwa wataieleza Marekani sheria hiyo inapinga tabiaambayo sio ya 
    kiafrika na maadili ambayo hayakubaliki katika jamii nyingi za 
    kiafrika.Serikali imesisitiza kuwa vikwazo hivyo havitakuwa na athari 
    kubwa kwa nchi hiyo na pia imekanusha madai ya mashirika ya kijamii 
    kuwatayari sheria hiyo imechochea ongezeko la dhuluma dhidi ya wapenzi 
    wa jinsia moja


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.