June 22, 2014

  • TAHADHARI – UTAPELI KUPITIA CRDB INTERNET BANKING



    Kuna Utapeli umeanza kusambaa saa chache zilizopita kupitia CRDB INTERNET BANKING .

    Anayefanya utapeli huu ametengeneza majina bandia ya watu maarufu kama wanasiasa na wanamuziki kisha anaingiza watu kwenye contact list yake halafu anawatumia ujumbe huu kama vile yeye ni mtu halisi .

    Mtu anapokubali anampa huyu jamaa taarifa zake za benki halafu mwisho wa siku hela zake zinaweza kuhamishwa kwa njia ya mtandao .
    MFANO WA UJUMBE NI HUU
    -----------------------------------------------------
    Habari za wakati ndugu watanzania! Kwa yoyote ambae amejiunga na huduma ya CRDB Bank kupitia Online. Internet Banking sio SIM BANKING alie jiunga na Internet Banking. Tafadhali naomba tuwasiliane kuna project maalum yenye faida kwangu nakwako pia kwa kushirikiana nao CRDB Bank. Malipo ni kila wiki katika hiyo project. Nitumie meseji inbox kama umejiunga na internet banking na unahitaji kushiriki katika hii project
    ==============================================================
    Mpaka sasa hivi nimegundua majina 2 ya Kala Jeremia ambaye ni mwanamuziki na Jerry Silaa ambaye ni mwanasiasa .
    Tuchukuwe tahadhari na tusambaze ujumbe huu .
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.