May 21, 2014

  • Makampuni yanayofanya Utafiti hii yahusu sana.



    Na Nathaniel Limu, Singida
    MAKAMPUNI yanayojishughulisha na tafiti mbali mbali za nafaka yameshauriwa kuongeza juhudi zaidi ili kupata mbegu bora zitakazowasaidia wakulima kupata chakula cha kutosha na kujikomboa kiuchumi.
    Wito huo umetolewa hivi karibuni na Diwani wa Kata ya Mwasauya (CCM) tarafa ya Ilongero wilaya ya Singida, Seleman Ntandu wakati akizungumza kwenye kilele cha sherehe za wakulima wa kata ya Ikhanoda na Mwasauya.
    Amesema ili kilimo kiweze kuwa na tija kwa wakulima hasa wakati huu ambao dunia inapambana na majanga mengi yanayosababishwa na tabia nchi, ni lazima watumie mbegu bora na zilizofanyiwa utafiti wa kina.
    mtama pic 6
    Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Namburi inayozalisha mbegu za mtama na uwele,Dk.Andrew Peter Mgonja akizungumza kwenye kilele cha sherehe za wakulima wa vijiji vya Ngamu na Mwasoiya wilaya ya Singida.Wa tatu kulia (waliokaa) ni Diwani wa kata ya Mwasoiya Selemani Ntandu na wa pili ni Mwenyekiti wa kijiji cha Mwasoiya.Picha zote na Nathaniel Limu.
    “Kwa hiyo, ndugu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Namburi inayozalisha mbegu za mtama na uwele nakuomba usichoke kufanya utafiti zaidi ili kampuni yako iweze kupata mbegu bora zaidi itakayowasaidia wakulima kuondokana na njaa na wakati huo huo wajiongezee kipato kwa kuuza mazao ya ziada”,alifafanua.
    Awali Mkurugenzi wa Kampuni ya kuzalisha mbegu za mtama na uwele ya Namburi ya mjini Arusha, Dk. Andrew Peter Mgonja amewataka wakulima kutumia mbegu za mtama na uwele zinazozalishwa na kampuni yake kwa madai kwamba zinakabiliana na ukame uliopo kwenye mikoa ya kanda ya kati.
    mtama 5 picsDiwani wa kata ta Ikhanonda jimbo la Singida kaskazini,ikitoa nasaha zake katika kilele cha sherehe za wakulima wa vijiji vya Ngamu na Mwasoiya.Pia aliwahamasisha kuboresha utengenezaji wa pombe ya kienyeji ya mtukuru ili ianze kuhifadhiwa kwenye chupa/pakiti ili iuzwe ndani na nje ya mkoa.
    Akiijengea nguvu hoja yake hiyo, amesema mbegu aina ya naco mtama one (1) ambayo tarafa ya Ilongero imeipa jina la Dk. Parseko Kone kwanza kwa eka moja inatoa gunia 13 ikilinganisha na gunia 4 za mtama wa kienyeji.
    mtama 3 pics
    Mkurugenzi wa kampuni ya uzalishaji wa mbengu bora ya Namburi,Dk.Andrew Peter Mgonja (kushoto) akikagua shamba darasa la kijiji cha Mwasoiya wilaya ya Singida.Kulia ni afisa kilimo wilaya ya Singida,Sankwera.
    “Naco mtama (1), inakomaa kwa kipindi cha miezi miwili tu wakati mtama wa asili unakomaa baada ya miezi sita. Ina soko kubwa kwenye makampuni yanayotengeneza bia na mabua yake yana mafuta ambayo yanayoweza kuendesha mitambo mbalimbali”, alifafanua Dk. Mgonja.

    mtama 4 picsWakulima wa vijiji vya Mwasoiya na Ngamu jimbo la Singida kaskazini,wakikagua shamba darasa la kijiji cha Mwasoiya ikiwa ni sehemu ya sherehe za wakulima wa vijiji hivyo.
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.