June 19, 2014

  • JUST IN: HUDUMA YA TRENI YA ABIRIA YA BARA KUANZA TENA JUMANNE JUNI 24, 2014




    JUST IN: HUDUMA YA TRENI YA ABIRIA YA BARA KUANZA TENA JUMANNE JUNI 24, 2014
     Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unafuraha kuwataarifu  abiria wote na wananchi kwa jumla  kuwa kutokana na kukamilika ukarabati wa daraja eneo la bonde la mto Ruvu mkoani Pwani huduma ya treni ya abiria itaanza upya hapo siku ya Jumanne Juni 24, 2014 kutoka Stesheni ya Dar es Salaam saa 11 jioni. Wananchi wanotaka kusafiri wafike stesheni zilizo karibu yao kwa ajili ya kukata tiketi kuanzia  Juni 19, 2014.

    Halikadhalika muda wa kuondoka treni kwa siku za Jumanne na Ijumaa kutoka Stesheni ya Dar kwenda Kigoma na Mwanza utakuwa saa 11 jioni na zile za kutoka Kigoma na Mwanza kuja Dar  katika siku za Alhamis na Jumapili ni saa 11 jioni  kutokea Kigoma na saa 12 magharibi kutokea Mwanza.
                                                                                             
     Tafadhali atakayesoma taarifa hii  amuarifu na mwenzake.
    Uongozi wa TRL unawapongeza wananchi kwa ujumula kwa ushirikiano na uvumilivu waliouonesha wakati wakisubiri kukamilika kwa kazi ukarabati wa njia ya reli.

    Imetolewa na Afisi ya Uhusiano ya TRL kwa Niaba ya
    Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ,
    Mhandisi  Elias Mshana
    Dar es Salaam,

    Juni 18, 2014.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.