May 19, 2014

  • Siri ya watoto kupotea, kuibwa yabainika

     
     
     
     
    Mkazi wa Kyela mkoani Mbeya, Mboka Mwakikagile (20) akiwa na mtoto wake Godluck Mwangosi katika Hospitali ya Rufaa Meta ya jijini Mbeya baada ya polisi kumkamata mtu anayedaiwa kumwiba mtoto huyo. Picha ya Maktaba
    Dar es Salaam. Kwa muda mrefu kumekuwapo na taarifa za watoto kupotea katika mazingira tofauti, huku baadhi yao wakipatikana na kuunganishwa tena na wazazi wao, lakini wengine hawajaonekana hadi leo.
    Wakati wazazi na walezi wa watoto hao wakiwa katika kiza kinene wasijue nini cha kufanya, serikali na wadau wanaoshughulikia masuala ya watoto bado hawajapata jibu la swali;watoto hao wapo wapi? Badala yake wameweka wazi sababu za watoto kupotea au kuibwa.
    Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika mikoa mbalimbali nchini kubaini sababu za watoto hao kupotea, umebaini kuwa baadhi ya watoto huondoka nyumbani baada ya kutokea ugomvi kati ya wazazi au walezi wao.
    Sababu nyingine ni kuibuka kwa biashara ya watoto wanaouzwa kwa watu ambao hawana watoto, nchini na nje ya nchi na imani za kishirikina zinazochochewa na waganga wa jadi.
    Taarifa kutoka polisi zinasema kuwa baadhi ya watoto walioripotiwa kwenye vituo vya polisi kupotea au kuibwa, walibainika kuchukuliwa na mmoja wa wazazi wa mtoto kutokana na migogoro kwenye familia.SOMA ZAIDI>>>>>>>>>
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.