May 14, 2014

  • ROY KEANE ASEMA PHIL JONES NA CHRIS SMALLING BADO SANA KUVAA JEZI YA MANCHESTER UNITED …haridhishwi pia na kuitwa kwao timu timu ya taifa




    Warned: Roy Keane has told Phil Jones (right) he needs to toughen up if he wants to make it at Man United
    NYOTA wa zamani wa Manchester United, Roy Keane amemuonya Phil Jones kuwa anahitaji kugangamala kama kweli anataka kuwa mchezaji tegemeo Manchester United.
    Jones alichukuliwa kama Duncun Edwards (beki nyota wa zamani wa United) wakati aliposajiliwa kwa pauni milioni 16.5 kutoka Blackburn Rovers mwaka 2011.
    Lakini Keane amedai beki huyo amepoteza muda mwingi kwa kuwa majeruhi kama alivyo mchezaji mwenzake Chris Smalling aliyesajiliwa mwaka 2010 kutoka Fulham kwa pauni milioni 10 ambaye Roy Keane anasema maendeleo yake yamekuwa yakirudi nyuma siku hadi siku.
    Unconvinced: Keane says the United duo need to do better if they want to cement a place at Old Trafford
    Keane alisema: “Tuliambiwa Jones atakuwa Duncan Edwards – Smalling atakuwa hivi na vile.
    “Nimetazama ‘live’ mechi kumi za United mwaka huu na wamekuwa hawana cha kufanana na hayo yaliyosemwa juu yao. Kama kuna chochote basi nadhani ni kwamba wamekuwa wakiporomoka.
    “Unasema unapaswa kuwapa wachezaji nafasi ili wakomae, lakini pia unakuwa na wachezaji ambao utawaambia, ‘Umepewa nafasi na umeshindwa kuitumia’. Wanapaswa kuongeza kiwango chao kama kweli wanataka kuwa nyota wa Manchester United.
    “Jones anahitaji kugangamala. Kila wakati nimekuwa nimekuwa nikiumuona akitolewa nje kwa kuumia.”
    Roy Hodgson amewachukua wachezaji wote hao wawili kwenye kikosi cha timu ya taifa cha England kitakachokwenda Brazil Kombe la Dunia wakitarajiwa kuwa suluhisho la mabeki wa kati iwapo Gary Cahill na Phil Jagielka watakuwa hawako fiti.
    Criticism: Keane believes Chris Smalling (left) has gone backwards in his development with Man United
    Alipoulizwa kama wachezaji hao ni wazuri kiasi cha kuwa mbadala wa mabeki wa kati, Keane aliongeza: “Sio kwa kiwango chao cha sasa. Wawili hao wamekuwa na msimu mbovu.
    “Lakini pengine England inaweza ikawahitaji, unaweza ukawa na majeruhi. Pengine kwenye nafasi zingine wanaweza wakahitajika. Labda hiyo ndio sababu kubwa ya Roy kuwachukua Jones na Smalling, kwa kujua kuwa wanaweza kucheza hata kama mabeki wa pembeni au kiungo.” 
  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.