May 15, 2014

  • MADOGO WA MANCHESTER UNITED WAVULIWA TAJI NA CHELSEA …wapigwa 2-1 kwenye fainali

     
    Match winner: Lewis Baker, who scored the decisive goal, at the centre of Chelsea's celebrations

    LEWIS Baker alikuwa shujaa wakati Chelsea ilipotoka nyuma na kuichapa Manchester United 2-1 na kunyakua kombe la Premier League kwa vijana chini ya miaka 21.

    Katika fainali hiyo iliyopigwa Old Trafford, kiungo huyo wa Chelsea alifunga bao la ushindi dakika ya 79 akitumia vizuri mwanya ulioachwa na mabeki wa United na kuuchonga mpira uliompita kipa Ben Amos.

    Winner: Baker (left) sweeps home the 78th minute winning goal for Chelsea

    Man of the moment: Lewis Baker wheels away to celebrates putting Chelsea in the lead

    LEWIS Baker akishangilia baada ya kufunga bao la ushindi

    Lilikuwa ni moja kati ya mabao matatu matamu yaliyofungwa katika fainali hiyo iliyowaburudisha vilivyo watamazaji 13,000.

    United ambao walikuwa wanatetea taji lao, walifunga bao la mapema kupitia kwa Tom Lawrence kunako dakika ya 12.

    Cool: Tom Lawrence (second left) opens the scoring with a left-footed shot past Jamal Blackman

    Opener: Lawrence (right) gave the United youngsters an early lead with a well taken strike

    TOM Lawrence furahani baada ya kuifungia bao United

    Chelsea wakasawazisha dakika 10 baadae wakati Mbelgiji hatari Charly Musonda alipowafungisha tela mabeki watatu wa United na kuachia shuti la chini chini lililotinga wavuni.

    Manchester United: Amos; Varela, McNair, M Keane, James (Blackett 81); Janko, Ekangamene, Pearson, A Pereira, Lawrence (Harrop 84); Wilson (Weir 67)

    Chelsea: Blackman; Ssewankambo, Aina, Christensen, Nditi; Loftus-Cheek (Palmer 77'), Baker, Ake; Swift, Feruz, C Musonda (Colkett 85')

    Hair raising: United's Ben Pearson (left) and Chelsea's Nathan Ake battle for the ball during the first half

     NYWELE hewani: Ben Pearson (kushoto) na Nathan Ake wa Chelsea katika heka heka nzito

    Watching on: Paul Scholes (left) and Ryan Giggs were in attendance at Old Trafford

     MAKOCHA Paul Schoes na Giggs wakitazama jahazi lao la United likizama

    Dejection: The Man United players stand and watch as Chelsea lift the trophy

     HUZUNI: United wakiangalia Chelsea wanavyokabidhiwa kombe

     

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.