May 15, 2014

  • ARSENAL YADHAMIRIA KUJARIBU KUMSAJILI BENZIMA KWA MARA YA TATU

     
     
     

    Target: Arsenal boss Arsene Wenger has failed with bids for Benzema in the last two summer transfer windows

    ARSENAL itaangalia uwezekano wa kumpata mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzima mara tu baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.

    Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa amekuwa akiwindwa na Wenger kwa miaka kadhaa ambapo Arsenal ilishindwa kumsajili mshambuliaji huyo katika vipindi viwili mfululizo vilivyopita vya majira ya kiangazi.

    On the move? Benzema has just 12 months left on his contract with Champions League finalists Real

    Arsenal wako tayari kujaribu tena kupata saini ya Benzima kiangazi hiki, ikiwa imedhamiria kuimarisha kikosi chake kwa kumpata mshambuliaji 'world class'.

    Benzima amebakiza miezi 12 kwenye mkataba wake jambo linalodhihirisha kuwa ni lazima aidha ajadili mkataba mpya wa kukipiga Real Madrid au auzwe. Kinyume na hapo ni kwamba nyota huyo ataondoka bure mwishoni mwa msimu ujao.

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.