May 11, 2014

  • ABRAMOVICH AANZA KUTENGENEZA ZENGWE LA KUMTIMUA MOURINHO CHELSEA

     

    Frustrated figure: Chelsea owner Roman Abramovich is reportedly unhappy with Jose Mourinho's brand of football

    CHELSEA kumaliza msimu bila taji lolote ni jambo lisilokubalika kwenye akili ya mmiliki Roman Abramovich.

    Soka lililokosa mvuto ni 'adui' miwngine wa Abramovich. malumbano ya kocha na wachezaji, kocha kukaripiana na waamuzi ni kero nyingine kwa tajiri huyo wa kirusi.

    Difficult start: Jose Mourinho has failed to win a trophy on his return to Stamford Bridge

    Yote haya yanatokea Chelsea chini kocha Jose Mourinho.

    Inasemekana Abramovich yupo tayari kufutialia mbali mapenzi yake kwa Mourinho na hata kumtimua.

    Abramovich alitarajiwa kuwepo uwanjani katika mechi iliyopita dhidi ya Norwich lakini akaingia mitini.

    Amekuwa na kawaida ya kufanya hivyo pale anapotaka kuchukua maamuzi magumu. Hata wakati anataka kumtimua Carlo Ancelotti alisusa kwenda uwanjani.

    Tajiri huyo anaona kama vile Mourinho haitendei haki himaya ya soka la kuvutia anayojaribu kuiejenga Stamford Bridge.

    Mshauri mmoja wa Abramovich anasema wachezaji kama Mata, Oscar, Hazard, Willian, Schurrle, Luiz na Azpilicueta ni aina ya wachezaji wanataka kutandaza soka lakini Mourinho amekuwa hawatumi katika mfumo mzuri na mbaya zaidi alimsotesha benchi Mata na hatimaye kumpiga bei.

    Gone: Mourinho was happy to let Chelsea favourite Juan Mata move to rivals Manchester United in January

    Hamtumii vizuri Luiz na pengine hatma ya mchezaji huyo iko mashakani.

    Wiki chache zilizopita, Chelsea ilipokuwa kwenye hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa, huku pia ikiwa kwenye nafasi ya kunyakua taji la Ligi Kuu, Abramovich alionekana kutojali mbinu za Mourinho, lakini baada ya kipigo cha Atletico Madrid na Sunderland kwenye uwanja wa nyumbani, kila kitu kikabadilika.

    Abramovich hana hamu tena na mbinu za Mourinho na lolote linaweza kutokea katika 'ndoa' hii ya pili ya wawili hao.

    The special relationship: Mourinho and Abramovich just the Portuguese's first appointment in 2004

    Mmiliki huyo ambaye mpaka sasa kishabadili makocha mara tisa tangu ainunue Chelsea mwaka 2004, huwa hapepesi macho katika kutoa maamuzi magumu.

    Abramovich amekerwa na faini aliyopigwa Mourinho kwa kosa la kitoto la kumkoromea refa katika mechi ya Sunderland iliyomaliza rekodi yake ya mechi 77 bila kufungwa Stamford Bridge.

    Je Mourinho ataonyeshwa njia ya kutokea? Ni jambo la kusubiri.

    Hawa ndio makocha waliopita Chelsea chini ya uumiliki wa Abramovich.

       Claudio Ranieri: 2004

       Jose Mourinho: 2004 - 2007

       Avram Grant: 2007 - 08

       Luiz Felipe Scolari: 2008 - 09

       Guus Hiddink: 2009

       Carlo Ancelotti: 2009 - 2011

       Andre Villas-Boas: 2011 - 12

       Roberto di Matteo: 2012

       Rafa Benitez: 2012 - 13

       Jose Mourinho: 2013 hadi sasa.

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.