September 01, 2014

  • UHAMIAJI KASUMULU YAJIPANGA KUDHIBITI EBOLA‏



    UHAMIAJI KASUMULU YAJIPANGA KUDHIBITI EBOLA‏
    Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme akizungumzia hali halisi ya mpaka na maandalizi ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.
     Barabara ya kuingilia Mpaka wa Kasumulu
     Hapa ni eneo la Tanzania kabla haujaingia katika Geti la Uhamiaji 
     Afisa Afya wa Mpakani Kasumulu, Ryoba Maijo  akielezea jinsi walivyojipanga kukabiliana na ugonjwa wa Ebola .
     Waandishi wa Habari wakiendelea kuchukua Taarifa Katika ofisi za Uhamiaji Kasumulu
     Shughuli mbalimbali zikiendelea upande unaounganisha Boda ya Tanzania na Malawi  
    Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme akionesha mpaka wa Tanzania na Malawi
     Hapa ni katikati ya Mpaka wa Tanzania na Malawi , Hapa waandishi wa habari  wakiuliza Maswali na kupata taarifa zaidi ya mpaka huo na Mwenyeji wao Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme
    Kikosi kazi cha Mbeya yetu Blog Kutoka kushoto ni Venance Matinya,Joseph Mwaisango na Fredy Anthony Njeje baada ya kazi kumalizika.
    ***********
    WAKATI kukiwa na hofu ya kuingia kwa ugonjwa wa Ebola nchi jirani ya Congo, Maafisa uhamiaji mipakani wamejipanga kuhakikisha hakuna mgeni atakayeingia nchini akiwa na dalili za ugonjwa huo.
    Hayo yalibainishwa jana na Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme, alipokuwa akizungumza na Mbeya yetu  kuhusu mikakati ya kudhibiti wageni wanaoingia nchini kutokuleta ugonjwa huo.
    Mndemi alisema yeye pamoja na maafisa wake wamejipanga kuhakikisha kila mgeni anayeingia nchini anakaguliwa vizuri kabla ya kuruhusiwa kuendelea na safari kwa kuangalia kama ana dalili zozote za Ebola.
    Alisema ingawa bado hawajapelekewa vifaa maalumu vya kupimia wageni wanaoingia nchini ili kuwabaini kama wanazo dalili za ugonjwa huo lakini wanatumia mbinu mbali mbali kulingana na uzoefu walionao maafisa ikiwemo kumwangalia mtu na kumhoji.
    Aliongeza kuwa hivi sasa Afisa anayegongesha stempu ni lazima ajiridhishe na maswali anayomuuliza mtu na sio kukimbilia kukagua hati yake pasipo kuangalia alikotoka na anakokwenda kama ndiko kuliko athirika na ugonjwa huo.
    Alisema Mpaka wa  Kasumulu unachangamoto nyingi na kubwa ni kuwepo kwa njia za panya nyingi jambo linalowawia vigumu maafisa kudhibiti uingiaji holela wa wageni ambapo alisema kuna mipenyo 30 ya kuingilia nchini kutoka Nchi jirani ya Malawi.
    Kwa upande wake Afisa Afya wa Mpakani Kasumulu, Ryoba Maijo,alisema  idara yake imejipanga kutokana na kuwepo kwa fomu maalumu ambayo mtu yeyote anayepita hapo atakuwa akijaza taarifa zake ambazo zitambaini kama ana maambukizi au hana.

    Alisema tangu ugonjwa huo kuripotiwa baadhi ya Nchi idara hiyo imekuwa ikichukua tahadhari kubwa ili usije ukaingia nchini kupitia mipakani hivyo kuwa makini na kila mgeni anayepita hapo.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.