Rais wa Serikali ya                Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na                Teknolojia IMTU (IMTUSO), (katikati), akizungumza katika                mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati                akitoa taarifa kwa umma kufuatia maagizo ya Tume ya vyuo                vikuu Tanzania (TCU) dhidi ya chuo cha IMTU. Kulia ni                Naibu Naibu Waziri wa Mikopo na Ruzuku wa IMTU, Benson                Lukwambe na Makamu wa Rais, Walter Nnko.
        Na Dotto Mwaibale
        WANAFUNZI wa Chuo                Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia IMTU wameiomba                Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kuunda tume maalumu                itakayoshirikisha uongozi wa wanafunzi kufuatia                utekelezaji wa maagizo waliyokiwekea chuo hicho ili                kukamilisha kwa muda uliopangwa.
        Akizungumza na                waandishi wa habari Dar es Salaam leo Rais wa Serikali ya                wanafunzi wa chuo hicho,IMTU (IMTUSO), Meekson Mambo                alisema wanafunzi wa chuo hicho wana wasiwasi kuhusiana na                muda wa miezi mitatu uliotolewa na  TCU kuhakikisha chuo                cha IMTU kimekamilisha masharti yote waliyopewa vinginevyo                kitafungwa.
        "Matatizo ya chuo                hicho ni ya muda mrefu hivyo kukiwa na kamati maalumu                itasaidia kushughulikia suala hilo haraka na kulitafutia                ufumbuzi badala ya kukifunga chuo hicho ambako kutaleta                athari kubwa katika masomo kwa wanafunzi" alisema Mambo.
        Mambo alisema TCU                iunde kamati ya muda itakayoshirikiana na uongozi wa chuo                uliopo sasa pamoja na uongozi wa wanafunzi waweze                kusimamia na kuhakikisha kuwa maagizo ya TCU yanatekelezwa                ili kutoa fursa kwa wanafunzi kuendelea na masomo huku                mapungufu ya muda mrefu yaliyopo yakiendelea kutatuliwa                kwani muda huo wa miezi mitatu waliopewa ni mdogo.
        Aliongeza kuwa endapo                uongozi wa chuo utashindwa kutekeleza maagizo ya TCU                hawaungi mkono hoja ya kufunga chuo badala yake kiwekwe                chini ya serikali au chuo kikuu kingine ambacho kina                kitakuwa na uwezo wa kusimamia mfano Chuo Kikuu cha Dar es                Salaa ambacho hakina kitivo cha afya.
        Makamu wa Rais wa                Serikali ya chuo hicho, WalterNnko alisema kukifunga chuo                hicho kutawaathiri wanafunzi zaidi ya 1000 waliopo chuoni                hapo.
        
0 comments:
Post a Comment