May 23, 2014

  • DAVID LUIZ WA CHELSEA KUTUA PSG KWA PAUNI MIL 50 …atakuwa beki ghali zaidi duniani

     
     
     
     

    Pointing to the sky: Chelsea star Luiz is on the brink of joining PSG in a deal costing close to £50 million

    DAVID Luiz wa Chelsea yuko njiani kutua Paris St Germain ndani ya masaa 48 yajayo katika usajili unaotegemewa kuwagharimu mabingwa hao wa Ufaransa kiasi kinachokaribia pauni milioni 50.

    Ingawa makubaliano halisi ya timu hizo mbili hayako wazi, lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 anatarajiwa kuwa beki ghali duniani akivunja rekodi ya Mbrazil mwenzake Thiago Silva na Marquinhos walionunuliwa na PSG kwa bei mbaya.

    Mara makubaliano yatakapofikiwa, PSG wataomba idhini ya kocha wa Brazil Luiz Felipe Scolari ya kumruhusu mchezaji huyo kuondoka kwenye kambi ya Kombe la Dunia kwenye kufanya vipimo vya afya.

    Tongue out: Luiz celebrates with the Europa League trophy after Chelsea beat Benfica in the 2013 final

    PSG wanaamini kuwa wanamnasa beki mwenye soka la aina yake  ambapo usiku uliopita walioneka kuwa tayari kulipa kitita wanachokihitaji Chelsea.

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.