June 23, 2014

  • SVEN-GORAN ERIKSSON ASEMA KAMA HODGSON ANGEKUWA KOCHA WA KIGENI ENGLAND, ANGETIMULIWA MARA MOJA



    SVEN-GORAN ERIKSSON ASEMA KAMA HODGSON ANGEKUWA KOCHA WA KIGENI ENGLAND, ANGETIMULIWA MARA MOJA
    SVEN-GORAN ERIKSSON ASEMA KAMA HODGSON ANGEKUWA KOCHA WA            KIGENI ENGLAND, ANGETIMULIWA MARA MOJA

    BAADA ya kuingoza England kwenye michuano ya kombe la dunia na kufanya vibaya kupindukia, kocha Roy Hodgson angetimuliwa kama angekuwa ni kocha wa kigeni.

    Hayo yamesemwa na kocha wa zamani wa England Sven-Goran Eriksson (pichani juu) ambaye aliikochi England mwaka 2001 hadi 2006.

    Lakini licha kufanya vibaya kuliko mara zote ambazo England imeshiriki World Cup, kibarua cha Roy Hodgson kipo kwenye mikono salama.

    Eriksson ameliambia  Sunday Telegraph kuwa kama angekuwa yeye ndiye aliyekwenda na timu ya England huko Brazil na kupata matokeo hayo, angetimuliwa mara moja.

    Hata hivyo Eriksson amesema Roy Hodgson ni kocha bora na England wanastahili kumbakiza.



  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.