June 19, 2014

  • WADAU WA SEKTA YA MAWASILIANO WAKUTANA ARUSHA



    WADAU WA SEKTA YA MAWASILIANO WAKUTANA ARUSHA
    IMG-20140618-WA0010
    Mwenyekiti wa umoja huo(EACO) Francis Wangusi ambaye pia ni  mkurugenzi mkuu  wa tume ya mawasiliano nchini Kenya
    IMG-20140618-WA0004
     Mkurugenzi mkuu  wa tume ya  mawasiliano nchini Uganda Patrick Mwesigwa
    IMG-20140618-WA0001
     Mkurugenzi wa  Watumiaji wa Watoa Huduma za Mawasiliano hapa nchini Dkt.Raynold Mfungahema
    IMG-20140618-WA0005
    Balozi Joseph  Bangurambona wa Burundi akiongea juu ya mkutano huo.
    IMG-20140618-WA0012

    Wadau  zaidi ya mia moja kutoka taasisi za mamlaka ya mawasiliano Afrika Mashariki (EACO} wamekutana jijini Arusha ili kuangalia namna ya kuweza kutatua changamoto zilizopo katika sekta hiyo muhimu ya mawasiliano.
     
    Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa umoja huo(EACO) Francis Wangusi  ambaye pia ni  mkurugenzi mkuu  wa tume ya  mawasiliano nchini Kenya alisema kuwa mkutano huo unalenga kujadili  changamoto zilizobainishwa na wadau wa sekta hiyo kuhusu vikwazo ambavyo vinakwamisha mbalimbali  usambazaji wa mawasiliano kwa nchi hizo.
     
    Wangusi alisema kuwa  sekta ya mawasiliano ina vitengo mbalimbali ikiwemo posta,mawasiliano ya simu na utangazaji na mitandao ya kijamii(internet) ambayo bado inakabiliwa na changamoto nyingi  zinazohitaji juhudi za wadau wa sekta hiyo ili kuwafikia watumiaji.
     
    Aidha alibainisha kuwa huduma ya posta bado inakabiliwa na changamoto ya anuani makazi ili kuwawezesha watumiaji  wanaoutumia huduma hiyo iweze kuwafikia kwa haraka kama zilivyo huduma nyingine.
     
    Hata hivyo wangusi aliongeza kuwa changamoto nyingine kubwa ni mawasiliano ya huduma za simu katika nchi za Afrika mashariki ambapo mbali na watoa huduma kupata faida kubwa lakini pia wanawatoza watumiaji gharama kubwa hivyo kupelekea watumiaji kutoka nchi moja hadi nyingine kushindwa kumudu.
     
    Kwa upande wake Mkurugenzi wa  Watumiaji wa Watoa Huduma za Mawasiliano hapa nchini Dkt.Raynold Mfungahema alisema lengo ni kuangalia kuwa mawasiliano yanawafikia watumiaji  na kufaidi huduma hiyo ya simu,internet,utangazaji na maswala ya posta.


    (Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.