Mshambuliaji                  wa Fiorentina Giuseppe Rossi ametemwa kwenye kikosi cha                  Italia cha wachezaji 23 ambacho kinajiandaa na fainali                  za Kombe la Dunia, licha ya kupona majeruhi ya goti.Rossi, 27, alicheza dakika 71                  katika mchezo wa Jumatatu uliomalizika kwa sare                ya 0-0 dhidi ya Jamhuri ya Ireland, lakini hakupata nafasi ya                  kwenda Brazil.Antonio Cassano amejumuishwa baada ya                kuifungia Parma magoli 12 msimu huu, wakati mshambuliaji                wa AC Milan Mario Balotelli ameteuliwa kwenye kikosi cha                Cesare Prandelli.
          Mabingwa hao wa Kombe la Dunia                mwaka 2006 wanaanza kampeni yao dhidi ya England Juni 12                na watakutana na Costa                  Rica na Uruguay kwenye Kundi B.
          Kiungo wa AC Milan Riccardo Montolivo                ametemwa baada ya kuvunjika mguu wake wa kushoto katika                mchezo dhidi ya Jamhuri ya Ireland.
          Wengine waliotemwa ni mshambuliaji                Mattia Destro, kiungo Romulo na walinzi Manuel Pasqual na                Christian Maggio.
          Kikosi kamili:
          Walinda mlango: Gianluigi Buffon                (Juventus), Salvatore Sirigu (Paris St Germain), Mattia                Perin (Genoa).
          Walinzi: Andrea Barzagli, Leonardo                Bonucci, Giorigo Chiellini (all Juventus), Gabriel Paletta                (Parma), Ignazio Abate, Mattia De Sciglio (both AC Milan),                Matteo Darmian (Torino).
          Viungo: Andrea Pirlo, Claudio                Marchisio (both Juventus), Thiago Motta, Marco Verratti                (both Paris St Germain), Daniele De Rossi (AS Roma),                Antonio Candreva (Lazio), Marco Parolo (Parma), Alberto                Aquilani (Fiorentina).
          Washambuliaji: Mario Balotelli (AC                Milan), Antonio Cassano (Parma), Alessio Cerci (Torino),                Ciro Immobile (Torino), Lorenzo Insigne (Napoli).
        
0 comments:
Post a Comment