October 15, 2015

  • MPIGA PICHA NA FAMILIA YAKE WAUAWA BURUNDI


    MPIGA PICHA NA FAMILIA YAKE WAUAWA BURUNDI
    Image copyrightGetty
    Image captionMaafisa wa polisi Burundi
    Mpiga picha wa runinga ya taifa nchini Burundi, pamoja na familia yake wameuawa katika mji mkuu Bujumbura.


    Polisi mjini humo wanasema kuwa walikuwa wakijaribu kuwaokoa maafisa wenzao wa polisi waliokuwa wametekwa nyara.
    Polisi wanasema kuwa watu kumi waliuawa katika kisa hicho akiwemo mpiga picha huyo wa runinga Christophe Nkeza-bahizi, mkewe na wanawe wawili pamoja na afisa mmoja wa polisi.
    Image captionWaziri wa usalama nchini humo Bunyoni
    Milio ya risasi na na milipuko ya mabomu yalisikika usiku kucha.
    Ghasia nchini Burundi, zilianza mwezi Aprili mwaka huu, baada ya Rais Pierre Nkurunziza kutangaza angewania muhula wa tatu wa urais.
    Katika miezi ya hivi karibuni, Burundi imekumbwa na wimbi la mauaji ya kiholela ya wanaharakati wa upinzani na maafisa wa usalama.
    Haijajulikana mara moja ni nani aliyewateka nyara maafisa hao wa polisi.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.