October 12, 2015

  • KANISA LA KKKT KUFANYA IBADA JUMAMOSI YA TAREHE 24 KUPISHA UCHAGUZI



    KANISA LA KKKT KUFANYA IBADA JUMAMOSI YA TAREHE 24 KUPISHA UCHAGUZI

    Na  Walter Mguluchuma
    Waumini wa Kanisa la Kiijili  la Kilutheli  Tanzania (KKKT)  Dayosisi ya Ziwa Tanganyika inayounda Mikoa ya Katavi na Rukwa imepanga kufanya ibada ya misa  Oktoba  24 badala ya  Oktoba 25 ilikuwapa nafasi waumini wa Kanisa hilo kushiriki uchaguzi mkuu utakao fanyika Jumapili ya oktoba 25



    Hayo yalisemwa hapo jana na Askofu wa KKT  Dayosisi ya Ziwa Tanganyika wakati alipokuwa akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu wakati akiwa Sumbawanga Mkoa wa Rukwa
     Alisema Kanisa limeamua  kuhamishia  ibada hiyo  siku ya juma mosi badala ya jumapili ili kutowa nafasi kwa waumuni wa Kanisa hilo kushiriki  kakamilifu uchaguzi mkuu wa Oktoba 25
     Kanisa  linatambua umuhimu wa uchaguzi Mkuu ndio  maana limehamisha shughuli zake zote ambazo zilikuwa zifanyike  jumapili ya Oktoba 25 na badala yake zitafanyika jumamosi ya oktoba 24
    Nae Katibu wa Dayosisi hiyo  Abrahamu Kombe amesema kuwa Kanisa limefanya jambo zuri sana kuhamishia  ibada siku hiyo ya jumamosi badala ya jumapili
     Alisema hakuna tena muumini wa Kanisa hilo Katika  Dayosisi ya Ziwa Tanganyika ambae atashindwa kupiga kura kwa kisingizio  cha kuwa   alikuwa kwenye ibada
     Mpaka saa kuna baadhi ya Madhehebu ya Dini mbalimbali  hapa nchini  wameishatangaza  kuhamishia  ibada zao siku ya jumamosi ya tarehe 24 badala ya tarehe 25 oktoba kwa ajiri ya kupisha uchaguzi mkuu utakaofanyika siku hiyo wa kuwachagua Wabunge na Madiwani na Rais


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.