October 15, 2015

  • WAATHIRIKA WA EBOLA WAOMBWA KUTUMIA KONDOM




    WAATHIRIKA WA EBOLA WAOMBWA KUTUMIA KONDOM
    Image captionKirusi cha ebola
    Waathiriwa wa ugonjwa wa Ebola wametakiwa kutumia mipira ya kondomu hadi kutakapokuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu matokeo ya utafiti yanayoonyesha kwamba virusi hivyo husalia katika majimaji ya mbegu za kiume kwa kipindi cha hadi miezi tisa.


    Shirika la afya duniani WHO limesema kuwa maambukizi ya ebola kupitia tendo la ngono ni kidogo mno na kutaja maeneo ya taifa la Sierra Leone ambayo yana idadi kubwa ya manusura lakini hayana visa vipya vinavyojirudia.
    Lakini mkuu wa WHO Margeret Chan ameiambia BBC kwamba kuna maswali mengi.''Hatujui iwapo wanaweza kuambukiza ama vipi ,bado hatuna ushahidi wa kutosha''.
    ''Kiwango cha ufahamu bado kinatutia wasiwasi ,ndio maana lazima tuchukue tahadhari ,kwa hivyo tunawashauri manusura kujilinda kupitia mipira''.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.